AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, wikiendi iliyopita, Wastara alifunguka kuwa kutokana na vitisho anavyotumiwa na ustadhi, hivyo akitua Dar kutoka mikoani atakwenda kumfungulia mashtaka kituo cha polisi kwani vitisho hivyo vinahatarisha usalama wake.
“Hebu fikiria mtu ananiandikia ujumbe kuwa atahakikisha nimeua ndiyo ataniacha, ina maana yale yanayonitokea ni yeye ananisababishia!” alisema Wastara.
Wastara alimtumia mwandishi ujumbe wa ustadhi huyo unaosomeka; ‘na bado siyo unatamani kuua na utaua, nitahakikisha umeua ndiyo na mimi nakuacha’.
Vitisho vya jamaa huyo vinakuja baada ya gazeti dada la hili, Ijumaa linalotikisa mitaani kila Ijumaa kuandika habari ya Wastara iliyosikitisha ambayo staa huyo alielezea namna anavyopatwa na hasira na kutaka kuua mtu ndipo ustadhi huyo akamjibu kwa ujumbe huo.
Ustadhi huyo aliwahi kuripotiwa na gazeti ndugu na hili, Risasi kuwa ana tatizo la kumsema Wastara hata awapo katikati ya swala, jambo lililomfanya awatafute waandishi ili wamsaidie kumuunganisha na mwigizaji huyo akitaka kumuoa lakini mwanadada huyo alidaiwa kumtolea nje.
GPL
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Nawe usilete karaha hapa
ReplyDeleteEda ilisha mwaka 47
Tafuta bwana
Mambo hapa Lowassa usitie kiwingu kilichojaa mavunde
Watu tuna likizo zetu ulaya Na USA kujibizana Na CCM
ReplyDeleteKwani hawati NGO