AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Lubuva ametoa kauli hiyo leo mchana ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuendelea na utangazaji wa matokeo ya Rais.
"NEC inapenda kuwatangazia wananchi kuwa kuhairishwa kwa uchaguzi Zanzibar hakutasababisha kuhairishwa kwa uchaguzi Tanzania.
"Uchaguzi wa Zanzibar unasimamiwa na ZEC na uchaguzi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzani unasimamiwa na NEC, ni katiba mbili tofauti
"Uvumi unaoendelea kwamba uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania umefutwa ni upotoshaji na si kweli, haujaathiriwa na lolote.
"Tuko hapa muda huu kuendelea na utoaji wa matokeo ya awali kama ambavyo tumekuwa tukifanya." Alisema Lubuva na kuendelea na zoezi la kutangaza matokeo hayo.
Msikilize Jaji Lubuva akiongea
UKAWA Wapigilia msumari
Akizungumzia sakata la uchaguzi mkuu kufutwa huko Zanzibar,Mwenyekiti mwenza wa Ukawa,James Mbatia amesema kuwa tume ya uchaguzi ZEC imeamua kuyafuta matokeo hayo baada ya CCM kushindwa vibaya.
"ZEC wameamua kuufuta uchaguzi mkuu Zanzibar kwa shinikizo la serikali ya Kikwete na CCM yake baada ya Maalim Seif Sharif Hamad kuibuka kidedea.
"Huwezi kufuta uchaguzi wa Zanzibar ukaacha uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano
"Unaposema Dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mujibu wa Katiba ni Tanganyika na Zanzibar
"Upande mmoja wa Jamhuri ya muungano umefuta uchaguzi, tena wametamka kufuta uchaguzi mkuu.Sasa kama upande mmoja umeshafuta, upande mwingine unasubiri nini?
"Huu ni mgogoro mkubwa. Kitendo cha Damian Lubuva kuendelea kutangaza matokeo ni sawa na kiini macho, anajifurahisha tu mwenyewe na ni kinyume cha katiba." Amesema James Mbatia
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK