Wakutwa Hai Baada ya Kufukiwa na Kifusi Mgodini Kwa Siku 41, Walikuwa Wakila Magome ya Miti na Chura

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

WATU watano waliokuwa wakichimba madini katika mgodi wa Nyangarata uliopo Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wamepatikana wakiwa hai baada ya kufukiwa na vifusi kwenye mashimo ya mgodi huo kwa siku 41.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Ofisa Habari wa Wizara ya Nishati na Madini, Badra Masoud amesema kuwa wachimbaji hao wanaodaiwa kuwa sita, walifukiwa na vifusi mnamo Oktoba 5, mwaka huu na kuendelea kuishi kwenye mashimo hayo huku wakila magome ya miti, vyura na udongo baada ya kushiwa chakula walichokuwa nancho, hadi jana Novemba 5, walipookolewa umbali wa kilomita 10 ndani ardhini na watano kati yao kukutwa hai huku mwenzao mmoja akidaiwa kufariki dunia.

Baada ya kupatikana wakiwa hai, manusra hao walikimbizwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Kahama ambako wanaendelea kupata matibabu.

Badra amewataja waliopatikana hai kuwa ni; Joseph Bulule, Chacha Wambura, Unyiwa Aindo, Msafiri Gerald na Muhangwa Amos. Wakati aliyefariki akimtaja kwa jina la Mussa Supana.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mungu ni mwema sana. Wasasihau kufanya ibada za shukurani kila mmoja kwa imani yake.

    ReplyDelete

Top Post Ad