Watumishi wa Afya Wanaomiliki Hospitali, Kliniki, Maduka ya Dawa Kuchunguzwa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

SERIKALI imetangaza kuwachunguza waganga na wauguzi, wanaomiliki hospitali, kliniki na maduka ya dawa baridi ili kubaini kama wanahusika na upotevu wa dawa kwenye hospitali za Serikali.

Akizungumza ofisini kwake juzi, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu alisema Desemba 26 alipotembelea Hospitali ya Ocean Road, aliamua kuunda kamati ya watu watano kuchunguza kama wanahusika na upotevu wa dawa hospitalini hapo na sehemu nyingine.

Alisema bodi ya hospitali hiyo aliyoiunda wiki mbili zilizopita, nayo imeshaanza kufanya kazi ya kubaini chanzo cha uhaba wa dawa hospitalini hapo.

“Hata ukisoma tamko langu, hatukatazi watumishi wa umma wa sekta ya afya kumiliki hospitali, kliniki au maduka ya dawa, lakini tunachoangalia ni namna gani tunaondoa mgongano wa kimasilahi,” alisema.

“Nimeenda Ocean Road, wagonjwa wanakufa kwa kukosa dawa, tusubiri kamati itoe taarifa.”

Alisema katika ziara yake aligundua madudu mengi ikiwamo pia fedha za bajeti ya dawa zilizokuwa zikipangwa kwa ajili ya hospitali hiyo, kutofika kwa wakati.

Waziri Mwalimu alisema asilimia kubwa ya wagonjwa wanaotibiwa hospitalini hapo ni maskini,na kwamba watu wenye uwezo hutibiwa katika hospitali kubwa za kulipia na wengine wanatumia bima ya afya.

“Kwa kuwanyima dawa wanaokuja hospitali hizi ni sawa na kuwanyanyasa,” alisema Waziri Mwalimu.

“Bajeti ya dawa inayopangiwa hospitali hiyo imeonekana nyingi zilikuwa hazifiki kwa wakati. Nimeshamuagiza katibu mkuu wa wizara yangu ahakiki kila fedha zinazopelekwa kwa ajili ya kununua dawa wizarani.”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Safi sana dadangu,mwendo ni ki-Magufuli magufuli tu,
    hapana cheza.

    ReplyDelete

Top Post Ad