AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mkazi wa kijiji cha Kalovya – Inyonga wilayani Mlele, Ramadhani Ally (20) amefariki dunia akipatiwa matibabu hospitalini baada kupigwa na kijana mwenzake.
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Dhahri Kidavashari amesema kuwa Ramadhani alifikwa na umauti baada ya kujeruhiwa na kijana mwenzake Ntema Kabembenya( 26), mkazi wa kijiji cha Ipwaga.
Kidavashari amesema tukio hilo lilitokea Januari 22, mwaka huu saa 12:55 jioni ambapo Ntema alimkuta Ramadhani (marehemu) akimtongoza dada yake (Ntemwa) mwenye umri wa miaka 12 (jina limehifadhiwa).
“Ntemwa alikasirishwa na kitendo cha Ramadhani kumtongoza dada yake mwenye umri wa miaka 12, alimshambulia Ramadhani kwa kumpiga na fimbo na kumjeruhi vibaya,” alieleza Kamanda Kidavashari.
Inadaiwa Ramadhani alikimbizwa katika Hospitali ya wilaya ya Mlele kwa matibabu lakini alifariki dunia siku iliyofuata akiwa anatibiwa.
Kwa mujibu wa Kidavashari, mtuhumiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi ambapo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK