AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Aliyekua mgombea Urais wa Chadema anayeungwa mkono na vyama vinavyounda UKAWA Mh.Edward Lowassa amelalamikia baadhi ya watendaji wa serikali kwa kuwaandama na kuwatisha wananchi na wafanyabiashara waliokuwa wanaunga mkono vyama vya upinzani na amezitaka idara zinazohusika kuchukua hatua ili kuepusha matatizo yasiyo ya lazima.
Akizungumza katika ibada maalum ya kukaribisha mwaka mpya iliyofanyika katika kanisa la kilutheri wilayani Monduli Mh Lowassa amesema amepokea malalamiko ya kuwepo kwa uonevu na vitisho kwa wadau walioonekana kuunga mkono vyama vya upinzani licha ya kuwa ni haki yao kikatiba.
Pia Mh Lowassa aliyekuwa mbunge wa jimbo la Monduli kwa tiketi ya (CCM) kabla ya kuhamia Chadema na kuwa mgombea urais amesema ataendelea kusaidiana na mbunge wa sasa Mh Julias Kalanga (Chadema) kutatua kero za wananchi na kuhakikisha kuwa misingi aliyoijenga inakuwa endelevu.
Kwa upande wao baadhi ya viongozi wa dini na wananchi waliohudhuria ibada hiyo wamepongeza uvumilivu wa kisiasa ulioonyeshwa na Mh Lowassa ambao umeendelea kuimarisha amani na utulivu nchini na wamewaomba wanasiasa wengine kuiga mfano huo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Tutoleeni s iasa taka. Rais tuliyenae anatutosha Mungu mlinde Rais wetu mpendwa JPJMAGUFULI.
ReplyDeletehiyo pete imekupendeza mzee
ReplyDeletePete za kikwete mikono yote
DeleteMbona hausemi
Wewe mwenyewe Fasidi mkubwa ni bora nenda kachunge
ReplyDelete