AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Agizo hilo lilitolewa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi Prof. Joyce Ndalichako, wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.
Alisema pamoja na serikali kutoa siku saba kwa baraza hilo kutoa sababu ya kuhama kutoka mfumo wa divisheni na kwenda katika mfumo wa GPA, bado baraza hilo limekuwa likitoa maelezo zaidi kuliko sababu za kuhamia mfumo huo.
Alisema hoja ya kuwa mfumo huo ulitokana na maagizo ya serikali haina nguvu kwa kuwa tayari baraza hilo ndilo linalotakiwa kubeba dhamana ya madaraja ya ufahulu.
Prof. Ndalichako alisema kutokana na bazara hilo kuendelea kutoa maelezo ambayo hayatoi sababu za kuhamia mfumo wa GPA, serikali imelitaka kufanya mapitio ya mfumo huo kwa lengo la kurudi katika mfumo wa awali wa divisheni.
Alisema baraza hilo linatakiwa kuweka viwango vya ufaulu kwa kuzingatia azma ya nchi kuelekea katika uchumi wa kati.
Aidha, Prof. Ndalichako aliitaka Necta kufuta karatasi ya pili ya watahiniwa wa kujitegemea ambayo imeanzishwa kama alama ya mtihani wa muendelezo wakati kiuhalisia ni mtihani wa mwisho.
“Wizara haiwezi kufikia azma yake ya kuelekea uchumi wa kati bila kuhakikisha viwango vya ufaulu vinawezesha nchi kutoa watalaamu wenye stadi na maarifa stahiki badala ya kuwa na wahitimu wengi wenye vyeti lakini hawakidhi mahitaji katika soko la ajira,’’ alisema.
Aliongeza kusema, wizara ina amini kuwa elimu ndiyo hazina ya nchi, hivyo itasimamia zaidi ubora wa elimu na kufuatilia kwa karibu kinachoendelea darasani ili kuhakikisha wahitimu wanakidhi matarajio na kuchangia maendeleo ya taifa.
Udaku Special Blog
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Tunaomba watoe huo mfumo wa GPA maana inatupa wakati mgumu kuelewa ufaulu halisi wa watoto wetu.
ReplyDeleteTunaomba watoe huo mfumo wa GPA maana inatupa wakati mgumu kuelewa ufaulu halisi wa watoto wetu.
ReplyDelete