Rais John Magufuli Arejesha Ikulu Kuwa Mahala Patakatifu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

John Magufuli
Mwaka mmoja uliopita ungeweza kuamini kuwa Mtanzania aliyetwaa tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani hatoitwa Ikulu na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya kupongezwa?

Jibu la swali hilo ni hapana; hasa ukizingatia kuwa wapo wanamichezo na wasanii waliotwaa tuzo ndogo zaidi lakini wakaalikwa katika ofisi kuu hiyo ya nchi kwa ajili ya kukutana na Rais.

Mwaka mmoja baadaye, Rais wa Tano John Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo halisi ya Watanzania na kufunga milango kwa wageni wasio na shughuli muhimu kwenda Ikulu, gazeti hili limebaini.

Ikulu pia imekomesha tabia iliyokuwa imezoeleka ya wageni kujazana kila siku sehemu ya mapokezi kwa ajili ya kwenda kuomba misaada mbalimbali kwa Rais, kama ilivyokuwa imezoeleka kwenye serikali iliyopita.

Gazeti hili lilifanikiwa kufika Ikulu sehemu ya mapokezi na kukuta viti vikiwa vitupu tofauti na awamu iliyopita ambapo mapokezi ya Ikulu ilikuwa ikitaka kufanana na eneo la shughuli hiyo katika hospitali yoyote ya mkoa nchini.

Viti vilijaa hadi kufikia hatua ya wageni hao kukaa kwa kupokezana.

Wakati leo ametimiza siku ya 80 tangu alipoapishwa Novemba 5, mwaka jana, Rais Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wachache muhimu, hali inayoashiria kuwa Ikulu sasa ni mahala patakatifu, kama ambavyo Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere alipata kuusia katika moja ya hotuba zake za kukumbukwa, ya Mei Mosi 1995 jijini Mbeya.

Miongoni mwa viongozi ambao Rais Magufuli amekutana nao Ikulu tangu aingie madarakani ni Sheikh Mkuu, Aboubakar Zuberi, Rais wa awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Rais wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na Kikwete.

Rais Magufuli pia alikutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein na Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Balozi Seif Idd kuzungumzia hali ya mkwamo wa kisiasa inayoendelea visiwani humo.

Wengine aliokutana nao kwa mazungumzo Ikulu hivi karibuni ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Katiba Mpya, Jaji Joseph Warioba, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Abdalah Bulembo, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Musa Jumma Assad na aliyekuwa Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Kutoalikwa Ikulu kwa Samatta ndiko kumedhihirisha kwamba sasa milango ya kwenda kumuona Rais haiko wazi sana kama ilivyokuwa kwenye awamu hiyo ya nne.

Rais Magufuli pia amepokea hati za mabalozi mbali mbali wanaoiwakilisha nchi zao ambao walifika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha.

Januari 7, Samatta alinyakua tuzo hiyo ya pili kwa ubora kwa wachezaji wa Afrika, baada ya Mchezaji Bora wa Afrika ambayo ilikwenda kwa Pierre-Emerick Aubameyang wa Gabon.
Tuzo hizo hutolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).

Kama Samatta angetwaa tuzo hiyo mwaka mmoja uliopita kwa mfano, isingekuwa rahisi kupita wiki moja bila Mbwana Sammatta kualikwa na Rais Ikulu.

Rais mstaafu Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa CCM,  ameshakutana na Samatta kwenye Ofisi Ndogo za chama hicho, Lumumba jijini.

Baada ya ushindi wake, Samatta alipokewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Wasanii, Nape Nnauye, ambaye alimpa gari lake atumie kwa muda pia.

Miongoni mwa wageni waalikwa wa mara kwa mara wa Kikwete Ikulu ni pamoja na mwanamuziki maarufu wa zamani Ray C ambaye Desemba 10, 2012 alikwenda kumshukuru kwa kumsaidia tiba ya matumizi ya madawa ya kulevya.

Habari ambazo Nipashe inazo, Ray C bado anaendelea kupata tiba ya kuacha dawa za kulevya katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Diamond Platnumz amewahi kualikwa mara kadhaa Ikulu, hata pale alipotwaa tuzo ndogo ambazo zilikabidhiwa kwenye hata klabu za usiku nje ya nchi.

Timu ya Azam imewahi kualikwa Ikulu baada ya kutwaa kwa mara ya kwanza Kombe la Kagame la Afrika Mashariki na Kati, taji ambalo Simba na Yanga zimelichukua jumla ya mara 11 katika historia.

Wachambuzi wa mambo walisema hali hiyo inadhihirisha kwamba Rais Magufuli amejikita katika kushughulikia matatizo ya msingi ya nchi, hasa vita dhidi ya ufisadi wa rasilimali za taifa, upatikaji wa huduma za jamii na uimarishaji wa miundombinu.

Dalili kwamba Ikulu sasa ni mahali patakatifu ilianza kujidhihirisha wakati wa kuapishwa kwa Baraza la Mawaziri mwishoni mwa mwaka jana.

Mawaziri hao waliapishwa bila mbwe mbwe wala shamra shamra kama ilivyozoeleka kwenye awamu ya nne, wahusika wakifika Ikulu bila kuambatana na utitiri wa ndugu na jamaa ambao chini ya Kikwete waliwalaki kwa maua na mashada baada ya kuapishwa.

Kwenye awamu ya nne, baadhi ya wateule walikuwa wakienda kuapishwa Ikulu na wake au waume zao, watoto, ndugu, majirani na jamaa zao na kupata fursa ya kupiga picha na Rais mara baada ya zoezi la kuapishwa.

Utaratibu huo umefutika baada ya Rais Magufuli kuonekana kujikita kwenye masuala ya msingi kama kupanga safu ya uongozi wake kwa kuwafuta kazi watendaji ambao anaona hawawezi kwenda na kasi yake.

Aidha, punde baada ya kuingia Ikulu Novemba 5, mwaka jana Rais Magufuli alifuta kitengo cha mapokezi ya wageni kwenye lango kuu la Ikulu na kuagiza watendaji wa serikali katika ngazi zote kutatua kero za wananchi mahala walipo ili kuwapunguzia usumbufu.

Kitengo cha Lishe kilichokuwepo Ikulu wakati wa serikali ya awamu ya nne kilivunjwa na watendaji wake kurudishwa kwenye Wizara mama walizotoka.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Duhh kweli magufuri sura ya kazi, ile yetu ya kucheka tupa kule kudadadeki hakuna muchezo

    ReplyDelete
  2. ile tabia ya wasani kwenda kupiga selfiee na rais ikulu hakuna tena

    ReplyDelete
  3. IKULU NI SEHEMU TAKATIFU NA ITAKUWA HIVYO FOR THE NEXT COMING 10 YEARS

    ReplyDelete

Top Post Ad