Tundu Lissu Atofautisha Tuhuma za Ufisadi za Lowassa na Profesa Muhongo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanasheria mkuu wa Chadema ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ametofautisha kilichomkuta Edward Lowassa kwenye sakata la Richmond na kilichomkuta Profesa Sospeter Muhongo kwenye sakata la Escrow bungeni.

Akiongea katika kipindi cha Mada moto cha Channel Ten, Lissu alieleza kuwa kwa kutumia ripoti za kamati za bunge zilizomhukumu Lowassa mwaka 2008 na ripoti za kamati ya bunge ilizomhukumu Profesa Muhongo mwaka 2014/2015 kuna utofauti mkubwa.

Alisema kuwa ripoti ya Mwakyembe ilieleza kuwa Lowassa anawajibika kwa makosa ya watu watano wa chini yake ambao aliwataja majina na kwamba hakuna sehemu ilimtaja Lowassa kuhusika moja kwa moja na sakata la Richmond.

Alisema kuwa kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyokuwa chini ya Zitto Kabwe na Deo Filikunjombe, ilieleza wazi kuwa Profesa Muhongo alishiriki kudanganya kuwa fedha zile hazikuwa za umma na baadaye ikabainishwa na kamati hiyo kuwa zilikuwa fedha za umma.

Kwa mujibu wa kamati ya Mwakyembe, Lowassa aliwajibika kwa sababu ya makosa ya hawa watu… Sasa hayo ni ya Lowassa. Yanalingana kiasi gani na ya Profesa Muhongo, yanalingana kiasi gani na ya Profesa Muhongo aliyesema kuwa bilioni 300 na ushee zilizotolewa Benki Kuu zikagawanywa kama njugu ni hela binafsi.

“CAG akachunguza akasema kuna hela za Umma, Takukuru wakachunguza hawajatuletea taarifa bungeni mpaka leo. Bunge likachunguza likasema hizi ni fedha za umma na hawa watu wawajibike na wakawajibishwa. Kuna ulingano gani hapo? Na hapo nazungumzia taarifa za kamati hizi mbili za bunge,” alisema Lissu.

Alikosoa uteuzi wa Profesa Muhongo akidai kuwa Bunge liliazimia kumfukuza na leo serikali inamrudisha kama vile hakuna kilichotokea hata kabla mwaka mmoja haujapita.

Udaku Special Blog
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Utamwamini vipi mtu aliediriki kula matapishi yake? Kama Lowasa hana hatia na makosa anayotuhumiwa basi Tundu Lisu na kundi zima la chadema ni watu waongo wa kutisha na ni watu wanaopaswa kuogopwa kama ukoma kwani ni wao hasa waliomuhukumu lowasa na kutaka kummeza dk mwakyembe mzima mzima kwa kutoa ripoti ambayo halingani na ufisadi uliopindukia wa mueshimiwa lowasa. Kumbuka mara tu mtanzania yeyote anapofungua kinywa chake na kusema fisadi basi sentensi ya pili itakayofuatia ni lowasa. Na Waasisi wa jina la fisadi kwa lowasa ni akina Lisu sasa leo unaposikia wananyanyua vinywa vyao wakijaribu kumsafisha lowasa kwa kweli inashangaza sana kama hawa watu kweli wapo serious na kauli zao. Kuhusu mohongo Tundu Lisu hana haja ya kumsemea zito kwani muheshimiwa zito angali hai na makini kuliko alipokuwepo chadema na alisha eleza wazi kwamba mwenye ushahidi juu ya kosa analotuhumiwa muheshimiwa mohongo aende mahakamani la sivyo,they have to shut up. Yeye Lisu si mwanasheria basi aache kuwadanganya watanzania kwenye vyombo vya habari vizuri angetumia taaluma yake kuwathibitishia watanzania mahakamani juu ya kosa la mohongo la sivyo aache kelele zisokuwa na mishiko ya aina yeyote. Na uzuri wa Dk Magufuli atafurahishwa sana na juhudi za Lisu za kumfichulia ufisadi wa mohongo kwani Magufuli kwake yeye ni kazi tu hapendwi mtu na alishaahidi ya kwamba mtumishi wake yeyote awe waziri au msambaza magazeti maofisini akihuska na ufisadi basi hatakuwa na kigugumizi cha kumchukuliya hatua kali kulingana na sheria.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kuma wewe koma Kama ulivyokoma ziwa la mamaoko
      CCM wezi wakubwa WA kura
      Ya Zanzibar mbona mmeufyata
      Muhongo nimshezi Saba Hana adabu kusema sisi Watanzania tufanye biashara ya kwa usomi gani
      Kama msomi ulaya au marekani wasimwachia ngo wangemlipa mara kumi ya mshahara aupatao bongo
      Mwizi tu

      Delete
    2. Huyu atakuwa muhindi koko
      Kajiweka karibu Na Muhongo ili apate ulaji
      Kweli Sofia simba alisema humwezi ngo
      Na mwaka huu jina lako halipi ngo

      Delete
    3. Huyu atakuwa muhindi koko
      Kajiweka karibu Na Muhongo ili apate ulaji
      Kweli Sofia simba alisema humwezi ngo
      Na mwaka huu jina lako halipi ngo

      Delete
    4. Pumbavu wewe
      Matapishi nyiye ccm mmezoea kula matapishi
      Mawaziri wamerudi au mzigo alikuwa rai WA awam ya nne
      Pro Tibaijuka
      Chenge
      Muhongo
      Magembe
      Na majizi
      Yote yamepwewa ubunge Na uwaziri

      Delete
  2. badala ya kuongea nafikiri sisi wana cdm tujipange upya tuangalie ni nini hasa tumekosea asiyekubali kushindwa si mshindani

    ReplyDelete

Top Post Ad