Hii ndio Hofu Kuu ya CCM Kwenye Uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es salaam....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ni wazi kuwa kila jicho la muumini wa demokrasia ,mpenda haki na mpenda maendeleo au mabadiliko limeelekezwa kwenye uchaguzi wa Meya wa Jiji hili linalosemekana kuwa ni jiji la maraha.....ukizingatia kuwa wapinzani (UKAWA) wana uhakika wa kumtoa meya kwa asilimia zaidi ya mia kutokana na wingi wa wapiga kura kwenye uchaguzi huo hivyo kuongeza msisimko zaidi kwenye uchaguzi huo....

Sarakasi zinazofanywa na serikali ya CCM kupitia mamlaka yao katika kuukwamisha uchaguzi huo zinazusha maswali mengi katika vichwa vya wapenda haki na waumini wa mabadiliko.....
Kiukweli ni miujiza pekee ndiyo itakayofanya CCM kuchukua kiti cha umeya mwaka huu kwa kutazama tu idadi ya wapiga kura(madiwani)..labda na ubabe ambao wameshauzoea kuufanya.....

Sasa swali la msingi ni kwamba ni kwanini hasa serikali ya CCM inaogopa jiji la Dar es salaam lote kuwa chini ya UKAWA....???

Jibu lake ni kwamba serikali ya CCM inaogopa kuwa UKAWA watakapochukua mamlaka za jiji lote la Dar es salaam ule Wizi wao, uchafu wao,Ufisadi wao na ukiritimba wao utakuwa bayana machoni mwa wananchi hivyo kuzidi kuwapa wakati mgumu zaidi katika nyakati zijazo za chaguzi mbali mbali hasa ikizingatia kuwa wananchi wa nyakati hizi kidogo wana uelewa wa mambo na uthubutu wa kuhoji mambo mbali mbali yanayo wagusa moja kwa moja....


Ni kichaa pekee ndiye asiyejua kuwa jiji la Dar es salaam ndio jiji linaloongoza kwa kukusanya mapato mengi zaidi kutokana na wingi wa watu na biashara mbali mbali zinazofanyika ndani ya jiji hili....lakini mapato hayo yanakutana na mchwa wengi wenye meno makali ya kutafuna visivyo halali yao.....hivyo kufanya hali ya mandhari ya jiji kutoendana na makusanyo yake...

Kutokana ufisadi na wizi wa mapato katika jiji hili imefanya jiji hili kuongoza kwa uchafu kila mahali hadi katikati ya jiji.....imefanya jiji hili kuwa na hali mbaya kiusalama hasa nyakati za usiku kutokana na kutokuwa na mataa ya mitaani...mabara bara mengi ya jiji hili hayapitiki hasa kipindi cha mvua kutokana na ubovu wake na miundombinu chakavu ya mifumo ya maji taka....yapo mambo mengi mabaya ambayo nikiyaa orodhesha hapa inaweza kuchukua hata masaa mawili...lakini mambo yote hayo hayaonekani na viongozi wa manispaa mbali mbali za jiji hili kwa kuwa vipaumbele vyao ni kuyatumikia matumbo yao na sio wananchi........

Habari njema ni kwamba UKAWA kupitia mipango na mikakati yao mizuri wanataka kuibadilisha hali hii ndani ya jiji hili....wanataka kuifanya Dar es salaam iwe na hadhi sawa na majiji mengine huko duniani....wanataka kuiweka Dar es salaam katika sura nyingine kabjsa.....wanataka Dar es salaam ipige hatua kutoka hapa ilipo jambo ambalo serikali ya CCM ililishindwa kwa kipindi chote cha uongozi wao...

Ninachowaomba wanaCCM ni kwamba lazima wajue kuwa nyakati zinabadilika hivyo wanatakiwa waendane na wakati...kama tuliwapa mamlaka kwa kipindi chote hicho na wakashindwa kutuondolea kero za jiji na ndio sie tulioamua kuwapumzisha kupitia masanduku ya kura tukitaka tuangalie pia uwezo wa wengine katika kutatua kero za jiji hili....hata wao wasipoturidhisha tutawapumzisha.....
Waache demokrasia ichukue mkondo wake....

Nawasilisha......

Chanzo:KikulachoChako
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad