Mabomu Ya Machozi Yarindima Jijini Mwanza Kuwatawanya Wananchi Waliotaka Kutoa Uhai wa Dereva Aliyegonga Mtoto

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi  jijini Mwanza wamewatawanya wananchi kwa mabomu katika eneo la Sinai, Mtaa wa Nyerere ‘A’ Kata ya Mabatini baada ya kutokea vurugu kutokana na mtu mmoja kugongwa na gari.

Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya watu hao wakati wakimuokoa dereva wa gari namba T. 520 CBM Mark X, Lifaty Dickson ambaye alimgonga mtoto wa miaka sita, Festo William.

Hatua hiyo ilifikiwa baada ya wananchi kuhisi kwamba polisi walitaka kumtorosha dereva huyo kwa madai ya kufanya ajali bila kukusudia.

Wananchi wanadai dereva huyo alifanya ajali baada ya kuendesha kwa mwendo kasi na hatimaye kumgonga na kumsababishia mauti motto huyo aliyekuwa Mkazi wa Kata ya Mahina.

“Mimi nilikuwa katika eneo hili la ajali ilipotokea, sasa huyu mtoto aliyefariki (Festo William) alikuwa anavuka katika eneo la watembea kwa miguu, zebra lakini huyu mwenye gari alishindwa kupunguza mwendo.

“Baada ya kuona hivyo sisi kama wananchi wapenda haki tulianza kumuadabisha huyu mtu lakini polisi wakaingilia kati na sisi hatukukubali,“ amesema shuhuda mmoja aliyetambulika kwa jina la Simon.

Justus Kamugisha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa, polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kumuokoa dereva wa gari hilo ambaye alikuwa akishambuliwa na wananchi.

Kamugisha amesema kuwa, polisi wake walishambuliwa kwa kupigwa mawe na wananchi hao, hivyo hawakuwa na njia yeyote ya kujiokoa tofauti na kutumia mabomu ya machozi.

“Polisi hawakuwa na njia yoyote tofauti na hiyo, waliamua kufanya hivyo ili kumuokoa dereva wa gari hilo na kuokoa raia wema wengine,” amesema Kamugisha na kuongeza kuwa watu watatu wanashikiliwa na polisi kutokana na mkasa huo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad