Mahakama Yasikitishwa na Hamaki za Steven Wasira Baada ya Kushindwa Kesi na Ester Bulaya Mpaka Kutaka Kumwagushia Mwandishi Kipigo..

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Uongozi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza umeelezea kusikitishwa na kitendo cha Waziri wa zamani wa kilimo, chakula na ushirika, Stephen Wasira kutaka kumshambulia mpigapicha wa gazeti hili, Michael Jamson na kumzuia kutimiza wajibu wake.

Akizungumzia tukio hilo juzi, Naibu Msajili Mwandamizi wa mahakama hiyo, Francis Kabwe alisema ofisi yake imesikitishwa na kitendo hicho kwani ni kuingilia uhuru wa vyombo vya habari katika kutimiza wajibu kwa jamii.

Hata hivyo, alisema mahakama haiwezi kuchukua hatua yoyote dhidi ya Wasira kwa sababu tukio hilo lilitokea nje ya chumba cha mahakama.

“Tukio hilo lingetokea mbele ya mahakama wakati shauri linaendelea ingehesabiwa kuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama na makahama ingechukua hatua, lakini kwa sababu lilikuwa nje ya mahakama, mikono yetu imefungwa labda vyombo vingine vinaweza kuingilia,” alifafanua Msajili

Alisema ushahidi wa picha zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vikimuonyesha Wasira akimkimbiza mpigapicha huyo ulimshtua, hasa ikizingatiwa umri na nyadhifa za kiserikali alizowahi kushika kiongozi huyo aliyedumu kwenye uwaziri tangu Serikali ya awamu ya kwanza.

Katika tukio hilo lililotokea Jumatano iliyopita, Jamson alinusurika kupigwa na Wasira aliyechukizwa na kitendo cha kumpiga picha, akiwa ameambatana na wadai katika shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Bunda. Wadai hao, Magambo Masato na wenzake wanne waliofika mahakamani hapo kusikiliza uamuzi wa mahakama kuhusu ombi la kukata rufaa kupinga shauri lao kutupwa, ambalo pia lilitupwa.

Akizungumza na Mwananchi juzi, Wasira alisema alilazimika kumuandama mpigapicha huyo baada ya kumpiga picha nyingi isivyo kawaida.

"Haiwezekani mtu anakupiga picha mia moja eti zote ni za habari? Najua fitna za uchaguzi bado zinaendelea na inawezekana huyu kijana anatumiwa na wanasiasa,” alisema Wasira

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad