AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumzia tukio hilo juzi, Naibu Msajili Mwandamizi wa mahakama hiyo, Francis Kabwe alisema ofisi yake imesikitishwa na kitendo hicho kwani ni kuingilia uhuru wa vyombo vya habari katika kutimiza wajibu kwa jamii.
Hata hivyo, alisema mahakama haiwezi kuchukua hatua yoyote dhidi ya Wasira kwa sababu tukio hilo lilitokea nje ya chumba cha mahakama.
“Tukio hilo lingetokea mbele ya mahakama wakati shauri linaendelea ingehesabiwa kuwa ni kuingilia uhuru wa mahakama na makahama ingechukua hatua, lakini kwa sababu lilikuwa nje ya mahakama, mikono yetu imefungwa labda vyombo vingine vinaweza kuingilia,” alifafanua Msajili
Alisema ushahidi wa picha zilizochapishwa kwenye vyombo vya habari vikimuonyesha Wasira akimkimbiza mpigapicha huyo ulimshtua, hasa ikizingatiwa umri na nyadhifa za kiserikali alizowahi kushika kiongozi huyo aliyedumu kwenye uwaziri tangu Serikali ya awamu ya kwanza.
Katika tukio hilo lililotokea Jumatano iliyopita, Jamson alinusurika kupigwa na Wasira aliyechukizwa na kitendo cha kumpiga picha, akiwa ameambatana na wadai katika shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi jimbo la Bunda. Wadai hao, Magambo Masato na wenzake wanne waliofika mahakamani hapo kusikiliza uamuzi wa mahakama kuhusu ombi la kukata rufaa kupinga shauri lao kutupwa, ambalo pia lilitupwa.
Akizungumza na Mwananchi juzi, Wasira alisema alilazimika kumuandama mpigapicha huyo baada ya kumpiga picha nyingi isivyo kawaida.
"Haiwezekani mtu anakupiga picha mia moja eti zote ni za habari? Najua fitna za uchaguzi bado zinaendelea na inawezekana huyu kijana anatumiwa na wanasiasa,” alisema Wasira
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Kubwa jinga ovyooo!
ReplyDelete