Talaka ya Jide Mazito Yaibuka!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Siku chache baada ya staa mwanadada mkongwe wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ kupewa talaka mahakamani na mumewe Gardner G. Habash ‘Captain’ mazito yameibuka baada ya kubainika uwepo wa hati nyingine ya talaka aliyoitoa Gardner kwa mwanamke mwingine, Risasi limeinasa.


Chanzo makini kimepenyeza habari kuwa mbali ya Jide anayetarajia kuibuka na kishindo kikubwa cha mabadiliko ya muziki wake hivi karibuni, Gardner alimpa talaka mahakamani mkewe wa awali aliyefahamika kwa jina la Idda Pius Mkunja, mwaka 2003.

“Mwenzangu Gardner anaonekana ndiyo kamchezo kake kumalizia ndoa mahakamani, ukiachana na Jide nimeona hati ya talaka nyingine aliyoitoa kwa Idda ambaye alimuona mwaka 1997,” kilisema chanzo hicho huku kikimpenyezea hati hiyo ya talaka (tazama pichani) mwanahabari wetu.

Kama hiyo haitoshi, chanzo hicho kiliweka wazi kuwa Gardner na Jide walishindwana miaka michache tu baada ya kufunga ndoa lakini waliendelea kuishi kwa imani kwamba wanaweza kuelewana lakini haikuwezekana.

“Hii ishu si ya miaka miwili iliyopita kama wengi wanavyojua. Ndoa ilikuwa na figisu muda mrefu sana, walishashindwana sema walifanya siri tu,” kilisema chanzo.

Baada ya kupewa hati hiyo, mwanahabari wetu alimtafuta Gardner ili aweze kuzungumzia suala hilo, simu yake iliita bila kupokelewa.

Chanzo: GPL
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad