Millard Ayo 'Mimi ni Miongoni Mwa Wanafunzi Waliofeli Kidato cha Nne Lakini Niliinuka na Kuendelea'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mtangazaji mahiri wa kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM Millard Ayo baada ya kufungua studio yake kubwa naya kisasa jijini Dar, ameanza kuuza vipindi vya burudani katika radio mbalimbali za Afrika Mashariki.
millard

Akizungumza Jumamosi hii katika mdahalo wa kuwatia moyo wanafunzi waliofeli kidato cha nne, ambao ulienda sambamba na uzinduzi wa video mpya ya Mrisho Mpoto, Millard alieleza mafanikio yake baada ya kupambana kwa muda mrefu.

“Nilijiuliza kwanini nisitumie uandishi wangu wa habari ili kusambaza habari Afrika?, ndipo nikaanza kujinyima ili nijenge studio yangu kwa pesa yangu mpaka imekamilika. Sasa hivi tayari nimeshaanza kuuza vipindi vyangu katika radio mbalimbali za Afrika, Kenya, Rwanda. Pia nimekuwa reporter wa radio mbalimbali za Afrika Mashariki, pia Nigeria kuna kazi maalum nimepata ambayo nimehifurahia sana,” alisema Millard.

Aliongeza, “Nimeona kama Rwanda na Kenya sasa hivi bongofleva ndiyo imetake over, hawa watu ingawa wanasikiliza muziki, pia wanataka stori mbalimbali za mastaa wa bongofleva. Kwa hiyo mimi nataka kuwaambia watu wangu tusikate tamaa kama ulianguka inuka endelea,”

Pia Millard Ayo alisema yeye ni miongoni mwa wanafunzi ambao walifeli kidato cha nne lakini aliinuka na kuendelea.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad