Wasaliti’ CCM waanza kutumbuliwa bila ganzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Huku kukiwa na taarifa kuwa wasaliti wa CCM wanaotarajiwa kutimuliwa wengi ni watu maarufu hasa viongozi wa ngazi za mkoa, tayari viongozi 21 wa Manyara, wameshatumbuliwa majipu bila ganzi.

Jumla ya viongozi 21, watatu wakiwa ni wa CCM Wilaya ya Babati Mjini mkoani Manyara na wengine 18 wa ngazi ya kata, wameshaadhibiwa na Mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete alichokiita kutumbua majipu bila aibu.

Inadaiwa kuwa viongozi hao walikuwa wanamshabikia aliyekuwa mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa.

Imedaiwa ushabiki ulisababisha CCM ipoteze jimbo na kata tano kati ya nane za Babati Mjini.

Katibu wa CCM mkoani Manyara, Ndeng’aso Ndekubali aliwataja waliofukuzwa uanachama kuwa ni wajumbe wa mkutano mkuu wa CCM Taifa, Cosmas Masauda, Zulekha Mohamed na mjumbe wa mkoa, Felix Kivuyo.

“Hawa wamefutwa uanachama baada ya kudaiwa kukisaliti chama kwa kuwapigia kampeni wagombea wa vyama vya upinzani na kuwaombea kura kwenye Uchaguzi Mkuu,” alidai Ndekubali.

Februari 24, mwaka huu, Kikwete alipokuwa akizindua nyumba ya chama hicho Kibaha mkoani Pwani, alisema mwanachama yeyote aliyekihujumu chama chao kwenye uchaguzi wa mwaka jana, atatumbuliwa jipu bila aibu.

Kikwete alikaririwa akisema tayari CCM ina majina ya wasaliti wote na mchakato wa kuwaadhibu unaendelea kuanzia ngazi ya matawi, kata, wilaya mkoa na Taifa. Alisema viongozi hao wamekiuka ibara ya 93, kifungu cha 14 ya Katiba ya CCM.

“Halmashauri Kuu ya CCM mkoa, imewavua nyadhifa viongozi 18 wa ngazi za kata wilayani Babati Mjini kwa kukiuka maadili, kushiriki ubadhirifu wa fedha na kukosa uaminifu,” alisema Ndekubali.

Alisema viongozi 18 wa ngazi ya kata ambao walivuliwa nyadhifa zao na kubaki kuwa wanachama wa kawaida, ni makatibu wa kata tisa, wenyeviti wa kata nane na katibu mwenezi mmoja wa kata, wote wa Wilaya ya Babati Mjini.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad