Mahakama Yamtia Hatiani David Kafulila....Yamwamuru Kulipa Faini Kwa Usumbufu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama Kuu Kanda ya Tabora inayoendelea mjini Kigoma, imemtia hatiani David Kafulila na kumtaka kulipa gharama kutokana na kukiuka kanuni ya kuwasilisha hati za kiapo mahakamani, zikiwa zimethibitishwa kama Sheria ya Makosa ya Uchaguzi inavyoelekeza.

Hata hivyo, kiwango cha faini anachotakiwa kulipa hakikutajwa. Kosa hilo halikuzuia ushahidi wake kupokewa upya mahakamani hapo.

Katika kesi hiyo aliyoifungua kupinga ushindi wa Hasna Mwilima (CCM) kuwa Mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila aliyegombea kwa tiketi ya NCCR Mageuzi analalamika kupokwa ushindi.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni Mwilima ambaye ni mshtakiwa namba moja wakati msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni washtakiwa namba mbili na tatu.

Jaji wa Mahakama Kuu, Ferdinand Wambali alisema Kafulila aliwekewa pingamizi na mawakili wa utetezi wakimlalamikia kuwasilisha hati ya kiapo iliyokiuka kanuni za uwasilishwaji kwa mujibu wa sheria.

Katika hoja yao mawakili hao waliiomba Mahakama hiyo kutozipokea hati hizo.

Jaji alisema Kafulila hakutekeleza matakwa ya kisheria ambayo yanaagiza anayewasilisha haki za viapo kuhakikisha kuwa zimethibitishwa kabla, kwa ajili ya shahidi kuanza kutoa ushahidi wake.

“Pingamizi la wajibu maombi linakubaliwa kwa upande mmoja, lakini pia linaachwa. Uamuzi wa Mahakama ni kwamba mleta maombi awasilishe upya hati za kiapo mbele ya Mahakama zikiwa zimethibitishwa,” alisema jaji.

“Lakini pia mleta maombi atalazimika kulipa gharama za usumbufu wa kesi kwa wajibu maombi kutokana na shauri kuahirishwa kwa siku mbili mahakamani.” Kufuatia mjadala huo kuwa mkali na mawakili wa kila upande kujenga hoja, jaji aliahirisha kesi hiyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad