Washindi wa Bahati Nasibu DKT Tanzania 'Fiesta Condoms' Warejea Kutoka Dubai

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Katika jitihada za kutangaza matumizi ya njia za uzazi wa mpango na kuzuia mimba zisizotarajiwa na magonjwa yanayo ambukizwa kwa kujamiiana (STDs) nchini, miezi miwili iliyopita katika siku ya wapendanao (valentine day), DKT International Tanzania shirika lisilo la kiserikali ambalo ni moja kati ya watoaji wakubwa wa bidhaa za uzazi wa mpango na afya ya uzazi nchini ilifanya uzinduzi wa aina mbalimbali za kondom zenye ubora zilizopewa jina la “Fiesta kondom” huko Bahari Beach Ledger Plaza hotel, Dar es salaam.

Wakati wa uzinduzi, shindano la bahati nasibu lilifanyika ambapo wanandoa watatu walishinda safari iliyolipiwa kila kitu ya kwenda na kurudi Zanzibar, Afrika ya kusini na Dubai.

Wakielezea msisimko wao wakati wa kurudi kutoka katika safari yao mwishoni mwa wiki katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), washindi wa safari ya kwenda Dubai ambao walitembelea Dubai kwa mara ya kwanza walifurahia wiki nzima ya kukaa na kutalii Dubai na Abu dhabi, waliishukuru DKT International Tanzania kwa kutimiza ahadi yao na kwa kuifanya safari yao kuwa ya kukumbukwa.
Katika mahojiano wakiwa uwanja wa ndege, washindi walisema kuwa safari imewapa fursa ya kutembelea sehemu za kusisimua huko Dubai kama Burj Khalifa, ambalo ni jengo refu kuliko yote Dubai, maduka makubwa ya kufanyia manunuzi pamoja na mashindano ya mbio za magari ya Formula one huko Dubai.

“Nimefurahia sana kupata safari hii ya kusisimua kwenda Dubai na mke wangu. Tuliweza kujionea wenyewe na kushuhudua mengi yanayoongelewa kuhusu jiji la maajabu. Ninapenda kuishukuru DKT International Tanzania kwa fursa hii nzuri na tunaahidi kuendelea kuwa mabalozi wazuri wa Fiesta kondom kila wakati ambapo tutahitajika kufanya hivyo. Alihitimisha bwana Justin Tinieshimo.



Kwa upande wake, Meneja Masoko wa Fiesta Kondom bwana Davis Kambi amesema “Tunafuraha kuhitimisha safari ya washindi wetu wa safari ya Dubai na wanashukuru kuwa na fursa hiyo ya kukumbukwa wakiwa Dubai.” Nyakati kama hizo ndizo ambazo zinahusu bidhaa ya Fiesta Kondom, kuleta wanandoa karibu katika nyakati za upendo; DKT International Tanzania imejidhatiti kulete wanandoa pamoja chini ya kampeni za Intimacy by Fiesta ambazo zitahakikisha wanandoa wengine wanapata safari ya kwenda katika sehemu za mbalimbali mwaka huu.

Bwana Kambi alitumia fursa hiyo kuhakikisha kuwa washindi wa zawadi ya safari ya kwenda Zanzibar tayari walisha kwenda na walisha rejea.

Aliwashukuru wote walioshiriki katika kuhakikisha kuwa shindano la bahati nasibu la uzinduzi wa Fiesta Kondom Valentine limefanikiwa. Fiesta Kondom itafanya tena tamasha la kukutana la wanandoa mwaka ujao ambapo wanandoa wataweza kushinda zawadi nzuri.

Bidhaa ya Fiesta Kondom ya DKT International Tanzania ilizinduliwa zaidi ya miaka 20 iliyopita na inapatikana katika nchi zaidi ya 40 duniani kote na sasa katika mikoa yote mikubwa ya Tanzania. Fiesta ina zaidi ya ladha 55 tofauti za kondom na zaidi ya aina 60 tofauti. Lakini kwa kuanzia DKT International Tanzania imetambulisha aina 5 tofauti; Fiesta Heat, Fiesta Ultra-thin, Fiesta Strawberry, Fiesta Max dotted and Fiesta Neon! DKT International Tanzania inapanga kuzindua aina zingine 3 za kondom zinazokamilishwa kwa utofauti wa aina mbalimbali kabla ya mwisho wa mwaka 2016.



MWISHO
Kuhusu DKT International Tanzania
DKT InternationalTanzania ni moja kati ya watoaji wanaoongoza wa bidhaa za uzazi wa mpango na afya ya uzazi Tanzania. Taasisi hii imekuwa ikifanya kazi zake tangia mwaka 2014. Katika mwaka 2015, DKT International Tanzania ilikuwa ni taasisi ya kwanza kufungua kiliniki maalumu kwaajili ya uzazi wa mpango, kliniki 3 za Trust Health & Wellness zinafanyakazi kwa sasa na ya nne itaanza kufanya kazi mwaka huu. DKT International Tanzania Inajengwa au kukamilishwa na mtandano wa wadau 30 wa Trust franchise katika mikoa 4.
DKT International Tanzania pia inatoa aina mbalimbali za bidhaa za kupanga uzazi zenye ubora wa hali ya juu kwa bei nafuu. Kutoa uchaguzi wa mbinu, kutambulisha teknolojia ya kibunifu na kuziba pengo katika mnyororo wa usambazaji ambao utasaidia kunusuru mahitaji. Ukichukulia idadi ya vijana wa Tanzania na kukua kwa matumizi ya uzazi wa mpango, DKT International Tanzania pia imeanzisha uwepo imara na wenye nguvu wa kidigitali na katika mtandao wa kijamii kuweza kuwafikia vijana. Kila mwezi zaidi ya watu laki moja wanafikiwa katika mtandao, na idadi hii inaendelea kukua kila mwezi.

Katika mwaka 2015, DKT International Tanzania iliuza zaidi ya kondom 670,608, 8,200 vifaa vya kupanga uzazi vya dharura, ana zaidi ya 18,000 za IUDs. Hii ni sawa na ulinzi wa wanandoa 225,600 kwa mwaka.


Kwa taarifa zaidi wasiliana na:-
Meneja Masoko wa Fiesta Kondom
Davis Kambi
Simu: 0652-687 800
Barua Pepe: davis@dkttanzania.org

Tafadhali pia Tembelea:-
Kondom chapa ya Fiesta Condoms
Facebook:  https://www.facebook.com/Fiesta-Condoms-TZ
Instagram:  turnonfiesta

Kondom chapa ya Bull
Tovuti:  www.kileleland.com
Facebook:  https://www.facebook.com/KileleLand
Instagram: kileleland

Chapa ya uzaizi wa mpango ya Trust
Tovuti: www.trustlife.co.tz
Facebook: http://www.facebook.com/Trustlifetz
Twitter: @trustlifetz
Instagram: trustlifetz
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad