CAF Yaiondoa Entente Setif ya Algeria, Kufuatia Ghasia za Mashabiki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

CAF
Shirikisho la soka barani Afrika CAF, limetangaza kuiondoa nje ya michuano ya klabu bingwa barani Afrika, klabu ya Entente Setif ya nchini Algeria, kufuatia ghasia zilizoonyeshwa na mashabiki wake wakati wa mchezo wa mwishoni mwa juma lililopita dhidi ya Mamelodi Sundowns ya Afrika kusini.

CAF, wamefuatilia mkasa huo na kujiridhisha kulikuwa na ghasia za makusudi zilizofanywa na mashabiki wa klabu ya Entente Setif, kwa kurusha vitu vyenye ncha kali, chupa za maji pamoja na miale ya moto katika sehemu ya kuchezea.

Kitendo hicho kilimlazimu mwamuzi kusimamisha mchezo kwa muda, kwa kuzingatia hali ya usalama kwa wachezaji, maafisa wa klabu zote mbili pamoja na mashabiki wengine ambao walikuwa katika hali ya utulivu.

Hata hivyo maamuzi hayo yanaipokonya ushindi wa mabao mawili na pointi tatu klabu ya Mamelodi Sundowns ambayo ilijitutumua na kufanikiwa kuibuka na ushindi katika uwanja wa ugenini.

Bado klabu ya Entente Setif ina nafasi ya kukata rufaa ya kupinga maamuzi yaliyochukuliwa na CAF dhidi yao
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad