Christian Bella atuzwa zaidi ya sh 15 milioni katika show ya ‘The Black Tie’ ya Wema Sepetu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkali wa masauti Christian Bella ameendelea kuonyesha ukongwe wake katika show ya ‘The Black Tie’ iliyofanyika Jumamosi hii katika ukumbi wa King Solomon jiji Dar es salaam.

Muimbaji huyo mwenye asili Kongo, alionyesha uwezo wake mkubwa wa kuimba hali ambayo iliwafanya mashabiki ambao walijitokeza katika show hiyo kutoa pesa zao mfukoni na kumtuza msanii huyo.

Akiwa mwenye furaha jukwaani, Bella alisema pesa ambayo ametuzwa jukwaani kwa usiku huo zinatosha kumpeleka Afrika Kusini na kushoot video mpya.

“Nashukuru mungu nimepata hela ya video, asanteni sana mashabiki wangu,” alisema Bella huyu akipiga magoti kumshukuru mungu.

Kwa upande wa muandaaji wa show hiyo, Wema Sepetu kupitia instagram yake, amempongeza msanii huyo huku akitaja kiwacho cha pesa alichotuzwa.

“7000$ alitunzwa jana Mzee wa Masauti… Jamani tusubirie Pictures eeh…. They are coming soo,” aliandika Wema.

Ukiachana na dola hizo, mashabiki wake wengine pamoja na wasanii wa filamu wakiongozwa na Steve Nyerere, JB pamoja na Irene Uwoya alishindana kumtuza msanii huyo.

Kiingilio katika show hiyo, kilikuwa ni tsh 50,000 kwa viti vya kawaida huku VIP iliwa tsh 100,000 na milioni 1 kwa meza nzima.

Chanzo:Bongo5
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pesa tulizotoa ni madafu halafu mama wa misifa anatangaza eti dola 7000!,acheni kujikweza ni upuuzi huo!

    ReplyDelete

Top Post Ad