AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akizungumza na vyombo vya habari leo katika kituo kikuu cha Polisi Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo Kamishna Simon Sirro, amesema Jeshi hilo limeanza rasmi oparesheni hiyo usiku wa kuamkia jana, ikiwa na lengo kusaka watu wanaoshukiwa kuwa ni majambazi wanaodaiwa kufanya matukio kadhaa ya ujambazi likiwemo lile la kuuawa kwa askari wanne waliokuwa wakienda lindoni, katika benk ya CRDB, Mbade jiji Dar es Salaam.
Amesema kuwa katika oparesheni hiyo kuna watu waliouawa na wengine wanashikiliwa na jeshi hilo, lakini amekataa kutaja idadi yoyote ile ya waliouawa au waliokamatwa kwa sababu za kiusalama kwa kuwa oparesheni hiyo bado inaendelea.
Kuhusu taarifa za uwepo wa askari aliyeuawa, Kamishna Sirro amekataa kuthibitisha au kukanusha na kusema kuwa taarifa kamili kuhusu oparesheni hiyo itatolewa siku ya Jumanne ya wiki ijayo.
Amewataka wananchi kuendelea kuwa watulivu, na kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo kwa kutoa taarifa zitakazoweza kufichua wahalifu hao na kusisitiza kuwa jeshi hilo litawabaini na kuwatia nguvuni wote waliohusika.
Katika hatua nyingine, Sirro ameendelea kupiga marufuku maandamano ya aina yoyote yale katika mkoa wa Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya zuio la jeshi la polisi la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa na maandamano nchi nzima.
Usiku wa kuamkia jana, hali ya taharuki iliwakumba wakazi wa Vikindu baada ya kikosi maalum cha askari kuvamia nyumba moja iliyoko eneo hilo, na kisha kuzuka kwa majibizano ya risasi kati ya polisi na wanaodaiwa kuwa ni majambazi waliokuwa katika nyumba hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK