Waziri Nape Avifungia Vituo Viwili vya Radio, Radio 5 Arusha na Magic Fm Dar

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametangaza kuvifungia kwa muda usiojulikana vituo vya Radio 5 ya Arusha na Magic FM ya Dar es Salaam kwa sababu za uchochezi.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Waziri Nape amesema kuwa vituo hivyo kwa nyakati tofauti zilitangaza habari ambazo ndani yake zina uchochezi.

“Adhabu hii ya kuvifungia kwa muda vituo hivyo viwili inaanza leo (Agosti 29 2016) hadi pale kamati itakapomaliza kazi yake,” alisema Nape.

Aidha, amesema kuwa ameiagiza Kamati ya Maudhui ya vyombo vya habari kuviita vyombo hivyo na kuvihoji kwa kina kisha kumshauri hatua zaidi ya kuchukua.

Waziri huyo ameeleza kuwa Serikali inaendelea kutambua mchango mkubwa wa vyombo vya habari katika kuleta amani na ushirikiano nchini na sio vinginevyo.

Hivi karibuni, Nape alitahadharisha kuwa vyombo vya habari vitakavyoripoti taarifa ambazo ni za uchochezi vitakumbwa na rungu la kuhusika kwa uchochezi pia.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

7 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Tutaona Mengi mpaka uongozi huu kumaliza MDA wake

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hongera sana Mh. Nape. Jukumu tumekupa na utekelezaji unao. Na tahadhari umeitoa na kuiweka Bayana. Sasa hawa wanojifanya Hamnazo wajaribu na Tutawashughulikia.

      Delete
  2. fala sana hy lapelape

    ReplyDelete
  3. Mtafunga magazeti, vituo vya habari, watu, then what. Huu ni woga wa ccm. Badala ya kujadili matatizo mbatumia nguvu.shows your weaknesses and fear in leadership.

    ReplyDelete
  4. Mtafunga magazeti, vituo vya habari, watu, then what. Huu ni woga wa ccm. Badala ya kujadili matatizo mnatumia nguvu.shows your weaknesses and fear in leadership.

    ReplyDelete
  5. Jamani Magic FM wamekosa nini? Alosikia hayo maneno ya kichochezi hebu atuambie tafadhali!

    ReplyDelete
  6. Hongera sana Mh. Nape. Jukumu tumekupa na utekelezaji unao. Na tahadhari umeitoa na kuiweka Bayana. Sasa hawa wanojifanya Hamnazo wajaribu na Tutawashughulikia.

    ReplyDelete

Top Post Ad