Barua ya Wazi Kwa Mwanamuziki Alikiba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wasalaam wakuu!
Sio siri uzalendo umenishinda haswaa! Yote ni juu ya Alikiba "Kingkiba" Maana mpaka sasa nashindwa kuelewa ni Nani aliyekuroga hadi unaendesha mziki wako kizaman sana.

Uliporudi na "Mwana" ilikuwa ni nyota njema na tumain jipya kwa sisi mashabiki wako dunian kote, Kweli hakuna anayebisha kwamba kuanzia "Mwana, Chekecha Cheketua, Nagharamia mpaka sasa "Aje" umefanikiwa kweli kweli kuzitingisha kuta za mabaazazi na mahafidhina wa Mziki wa Bongflava waliotaka kujimilikisha mziki kwa kujifanya miungu watu, Kwa hilo nakupa pongezi.

Ni ukweli uliowazi kuwa umerudi na Kasi ya "4G" ila ubaya ni 4G inayosoma "H", Alikiba sisi fans wako umeendelea kututesa kwa muda mrefu sana hasa kwa mambo yako unayofanya sisi hayatupendezi kabisa, Nilitaka waraka huu uwe wa siri ila mbinu zote hizo zimeshindikana. Na haya yafuatayo ni miongoni mwa mambo yanayotutesa sisi washabiki zako.

1. UKOSEFU WA COLLABO ZA KIMATAIFA, maana tangu ujinasibu kuwa una collabo na fally pupa na wasanii wengine wakubwa ni miaka imepita, Kweli Alikiba wewe ni wa kutupa collabo za wakina Nuh mziwanda, Abbyskilz, Dayna nyange, ommy dimpoz, Hapa najiuliza target yako hapo ni market ipi? Ali mbona unatutesa kiasi hiki?For How long we gonna wait?

2. PAGE ZAKO KWENYE SOCIAL MEDIA ZINABOA SANA, Mi nachofahamu social media ni sehemu adhimu na muhimu sana ya mafans kuwasiliana na msanii wao, kwa kupata updates mbalimbali, ila kwako hili suala limekuwa kinyume, Acc zako mfano Instagram 70% ya posts zako ni birthday za watu, kazi zako hatuon kabisa ukipost, Pia msanii gani muda mwingine unakaa week nzima bila kupost kitu kabisa, Unataka fans wako wafanyaje?

3.MSIMAMO WAKO KUHUSU TUZO, hapa napo tunashindwa kukuelewa je unataka tuzo au hautaki? Tangu mwaka umeanza tumeshuhudia ukipata nominations za tuzo mbalimbali Africa( Afrimma, UEA awards, Afrima Nigeria, AEUSA,AYCA Awards, African Oscar awards etc) lakin hata siku moja hatujawah kuona ukiripost au kuapreciate hicho kitu, mfano mwezi August ulishinda tuzo 2 za #AfricanOscarChoiceAwards lakini cha ajabu umekausha hadi leo kurepost hicho kitu, hapa sasa tunabaki njia panda, je unadharau waandaaji wa tuzo au sisi fans wako tuliokesha tukikupigia kura? Hapa tunaomba majibu au tupotezee kukusuport kwenye tuzo.

4: UCHELEWESHAJI WA PROJECT ZAKO, Hapa napo Alikiba umekuwa jipu sugu, tunashindwa kuelewa je tatizo ni wewe au management yako? Porojo na ahadi zimekuwa nyingi bila vitendo, Tunahitaji majibu ya kutosha zaidi tunataka tuone tofauti ya msanii wa Sony global music na wasanii wa mchangani

5. USIRI KATIKA MIKATABA NA MALI ZAKO, Hapa napo ndio kumekuwa na jipu sugu lenye ukungu kabisa, Sababu mara nyingi umekuwa ukiulizwa maswala adhimu kuhusu profit unazopata kutokana na mikataba yako ya Sony music na endorsement unazopata kama ubalozi wa Wild aid, ubalozi Jam food nutrition, Mali unazomiliki etc, Lakin umekuwa na kigugumizi kujibu, Mashabiki zako tuna kiu ya kusikia msanii wetu ananufaika vipi na mziki wake, na hili pia ni haki yetu ya msingi. Tuna mengi sana ila kwa leo tuishie hapa.

Imeandikwa na Shardcole
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad