AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hiyo ni baada ya kuondolewa kwa makato mengine yote muhimu kwenye mapato ya jumla ya mchezo huo ulioingiza Sh. Milioni 320 Simba na Yanga zikitoa sare ya 1-1.
Habari za ndani ambazo BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE imezipata zinasema kwamba, fedha hizo zimezuiwa kwa maelekezo ya Serikali kufuatia uharibifu uliojitokeza katika mchezo huo wa Oktoba 1, mwaka huu mashabiki wa Simba wakivunja viti.
Tokeo la picha la SIMBA WAVUNJA VITI
Na taarifa zinasema kwamba Serikali imezuia fedha hizo hadi hapo uchunguzi utakapokamilika juu ya hasara iliyojitokeza, ambayo kimsingi Simba wamekubali kulipa.
Habari zinasema mchezo huo uliingiza Sh. Milioni 320 wakati uharibifu uliofanywa na Simba unakaribia kuwa wa Sh Milioni 400.
Makato ambayo yamekwishaondolewa kwenye mapato hayo ni pamoja na asilimia18 ya VAT, asilimia 15 ya gharama za Uwanja, asilima 9 ya Bodi ya Ligi, asilimia 5 ya TFF, asilimia 3 ya DRFA na asilimia 8 ya gharama za mchezo.
Wenyeji Yanga SC wanastahili kupewa asilimia 40 ya mapato hayo wakati asilimia 20 ni za waliokuwa wageni, Simba SC.
Tayari Simba SC wameandika barua TFF kuomba wapatiwe mgawo wao wa mchezo huo kwa kuwa wanahitaki fedha za kujiendesha kwa wakati huu na deni hilo watalipa taratibu.
Hatua hiyo inakuja kufuatia mashabiki wa Simba kufanya vurugu Uwanja wa Taifa Oktoba 1, baada ya Yanga kupata bao la kuongoza dakika ya 26 lililofungwa na mshambuliaji Mrundi, Amissi Joselyn Tambwe katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara.
Bao hilo lilizua kizaazaa, wachezaji wa Simba wakimvaa refa Martin Saanya wakidai mfungaji, Tambwe aliushika mpira kabla ya kufunga. Na katika vurugu hizo, Saanya alimtoa kwa kadi nyekundu Nahodha wa Simba SC, Jonas Mkude dakika ya 29 kwa sababu ndiye aliyekuwa mstari wa mbele.
Kwa hali hiyo, mchezo ukasimama kwa takriban dakika tano baada ya mashabiki wa Simba kuanza kufanya vurugu waking’oa viti na kutupa uwanjani. Polisi walitumia milipuko ya gesi za kutoa machozi kuwatuliza mashabiki hao na mchezo ukaendelea hadi Simba SC wakasawazisha dakika ya 87 kwa bao la Shizza Kichuya. Lakini tayari TFF imeipiga Simba SC faini ya Sh. Milioni 5 kwa kosa hilo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK