Wanafunzi Wakumbwa na Ugonjwa wa Kuanguka Ovyo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wanafunzi wa kike 12 wanaosoma Shule ya Msingi Nditi, Wilaya ya Nachingwea, mkoani Lindi, wamekumbwa na ugonjwa wa kuanguka ghafla na wengine kupoteza fahamu, walipokuwa wakicheza katika viwanja vya shule hiyo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Amon Livigha, alikiri kutokea tukio hilo katikati ya wiki iliyopita, saa mbili asubuhi.

Alisema baada ya tukio hilo, baadhi ya wazazi walifika shuleni hapo na kuwachukua watoto wao na kwenda nao nyumbani.

“Nilipata taarifa ya kuanguka kwa wanafunzi hao nikiwa darasani nafundisha, hivyo kutokana na uzito wa tatizo, nililazimika kukatisha masomo na kwenda kuwahudumia watoto hao.

“Wakati tukiendelea kufanya utaratibu wa kuwakimbiza wanafunzi hao kituo cha afya kupatiwa huduma, baadhi ya wazazi walikataa watoto wao wasipelekwe hospitali na kuondoka nao,” alisema.

Mwalimu Livigha alisema kutokana na tukio hilo, kamati ya shule, wazazi na uongozi wa Serikali ya kijiji na kata hiyo wamekutana kujadili suala hilo.

Mtendaji wa kata hiyo, Juma Mng’anga, alikiri kutokea tukio hilo na kueleza kuwa tayari wameshatoa taarifa makao makuu ya wilaya, Nachingwea.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad