MGOGORO CUF, Pro Lipumba Azomewa na Wananchi Mkoani Lindi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) anayetambuliwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Prof. Ibrahim Lipumba amekutana na wakati mgumu baada ya wananchi wilayani Ruangwa mkoani Lindi kumzomea.

Prof. Lipumba alikumbana na hali hiyo alipokuwa mkoani humo katika ziara aliyoeleza kuwa ni ya kujenga chama. Akiwa anapita katika barabara huku gari lake likilindwa na vyombo vya ulinzi, wananchi waliokuwa wamesimama kando kando ya barabara walisikika wakiimba wimbo “Hatumtaki”, huku wengine wakimuita msaliti.

Mbali na wananchi hao waliokuwa wakimzomea, wengine walikuwa na mabango yaliyokuwa yakisomeka “CUF kwanza Lipumba baadaye”, “Hatukutaki msaliti wewe.”

Wakati hayo yote yakiendelea, Prof. Lipumba na viongozi wanaomuunga mkoani walikuwa ndani ya gari na hawakusema jambo lolote.

Kwa muda sasa kumekuwa na mgogoro wa uongozi ndani ya chama hicho kuhusu nafasi ya Mwenyekiti ambapo baadhi wanamtambua Prof. Lipumba kama mwenyekiti halali huku wengine wakumtambua Julius Mtatiro kuwa ndiye mwenyekiti halali.

Licha ya Prof. Lipumba yeye kuendelea kufanya mikutano ya ndani huku akipata ulinzi wa vyombo vya dola, Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif alizuiwa kufanya mkutano wa ndani uliokuwa umepangwa kufanyika mkoani Mtwara.

Itazame hapa chini video ya wananchi hao wakimzomea Prof. Lipumba.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad