AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Augustino Mtitu alishambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng'ombe wasiharibu mazao shambani kwake, Kipande cha mti kinachoonekana hapo mdomoni ndiyo mkuki uliokatwa ili kupunguza urefu wa mkuki huo wakati wakimkimbiza hospitali, Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa.
WITO KWA SERIKALI.
Ofisi Ya Mbunge Mikumi inatoa wito kwa Serikali kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki cha kinyama kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuweza kukomesha vitendo hivi vya kujichukulia sheria mkononi inayopelekea kuongezeka kwa uvunjifu mkubwa wa Amani na migogoro isiyokwisha kati ya wakulima na wafugaji wilayani KILOSA.
Imetolewa na:-
Robert A. Galamona
Katibu Ofisi Ya Mbunge
Mikumi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Unyama wa hali kubwa. Lini Serikali yetu itachukua majukumu kuondoa tatizo hili. Ni elimu tu inatakiwa hapa. Usalama wa raia ni kitu kikubwa sana. Angefanyiwa mtalii, mzungu Serikali ingehangaika kumchukulia ndege sababu ingebanwa. Kwa nini WAtanzania tunakubali na kuwa kimya mwenzetu anapovamiwa. Kwa nini tusiishike serikali kutujali. Elimu kwa wananchi kuhusu kuua, kupora, kutumia mapanga. Hii inabidi mhusika anyongwe mara moja ili watu waishi kwa amani. Sheria zinawabana wasio na hatia, wenye hatia hawachukuliwi sheria vipasavyo. Hii ni aibu kwa nchi na inabidi uongozi ujitafakari. Mtanzania hana Thamani mpaka awe tajiri au kiongozi wa siasa au ndugu zao?Lini tutajithamini wenyewe.
ReplyDelete