AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
DA
ES SALAAM: Baada ya juzikati kupatikana taarifa kuwa mwanamuziki,
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amepatana na baba yake mzazi, Abdul
Juma, inadaiwa kuwa katika sherehe ya kutimiza siku 40 ya mtoto wa
Diamond aitwaye Nillan ‘Chibu Junior’, babu mtu huyo naye atatinga
Sauzi.
Kwa mujibu wa ndugu wa karibu wa Diamond
aliyeomba hifadhi ya jina lake, baba Diamond ni kati ya watu
watakaopata nafasi ya kukwea pipa kwenda Sauzi kwenye tukio hilo
linalotarajiwa kuchukua nafasi Januari 16, mwaka huu.
“Sherehe
ya kumtoa Nillan inatarajiwa kufanya Johannesburg, kule kwenye mjengo
wa Diamond. Watu kadhaa kutoka Bongo wakiwemo mastaa wamepewa mualiko na
utakuwepo usafiri maalum wa ndege wa kwenda na kurudi Sauzi.
“Nilimsikia Diamond akisema hata mzee Abdul atapata fursa ya kwenda kuwaona wajukuu zake, kwa hiyo tusubiri tuone,” alisema mtoa habari huyo.
Katika kuweka uzani wa habari hii,
mwandishi wetu alifanya jitihada za kumpata Diamond lakini simu yake
haikuweza kupatikana mara moja.
Ijumaa lilipata fursa
ya kuzungumza na baba Diamond na kuulizwa kama ana taarifa juu ya safari
hiyo ambapo alisema: “Hata mimi nasikiasikia ila kama itakuwa hivyo
litakuwa ni jambo zuri kwani nitapata nafasi ya kuwaona wajukuu zangu.
Kama nilivyosema, mimi na Diamond hakuna shida tena kwa hiyo hata hilo
la kwenda Sauzi linawezekana kabisa.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Hivi huyu alienda South? 40 ya mtoto wa Diamond si ilikuwa jana
ReplyDeleteAwamu ya tano hii mkuu si ya ki-sport spot
Delete