Hatarii:Mtoto wa Miaka Mitano Afariki Dunia kwa Kukeketwa na Bibi Yake..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MTOTO mchanga wa siku tano amefariki dunia baada ya kufanyiwa kitendo cha ukeketaji na bibi yake aliyejulikana kama Longida Naingola mkazi wa Kijiji cha Naibera, wilayani Simanjiro, Mkoa wa Manyara.


Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Wilbroad Mutafungwa, kichanga hicho kutoka kabila la Wamasai kilifanyiwa kitendo hicho cha kikatili Desemba 30, mwaka jana katika Kijiji cha Naibera, wilayani Simanjiro.

“Mtoto alizaliwa Desemba 25, 2016 na Desemba 30, 2016 saa 4:00 asubuhi, bibi huyo alimkeketa na baada ya kitendo hicho hali ya mtoto ilikuwa mbaya kutokana na kutokwa na damu nyingi sehemu zake za siri,” alisema Mutafungwa.

Mutafungwa alisema ilipofika Januari 11, 2017 mtoto huyo alifikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC akiwa na mama yake mzazi, Fatina Joshua (14).

Alisema baada ya kufikishwa hospitalini hapo madaktari waliompokea walimkagua na kukuta mtoto huyo akiwa ameharibika vibaya sehemu zake za siri na ilipofika Januari 13, mwaka huu alifariki dunia.

Kamanda Mutafungwa, alisema baada ya kupata taarifa hiyo waliwatafuta watuhumiwa na kumkamata bibi pamoja na mama wa kichanga hicho.

Alisema mwili wa kichanga hicho umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC huku uchunguzi ukiendelea ili kuchukua hatua zaidi za kisheria.

Aidha, Kamanda Mutafungwa alisema jeshi hilo pia linaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Manyara kutokana na tukio hilo kufanyika huko.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad