AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
MTOTO mchanga wa siku tano amefariki dunia baada ya kufanyiwa kitendo
cha ukeketaji na bibi yake aliyejulikana kama Longida Naingola mkazi wa
Kijiji cha Naibera, wilayani Simanjiro, Mkoa wa Manyara.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro,
Wilbroad Mutafungwa, kichanga hicho kutoka kabila la Wamasai kilifanyiwa
kitendo hicho cha kikatili Desemba 30, mwaka jana katika Kijiji cha
Naibera, wilayani Simanjiro.
“Mtoto alizaliwa Desemba 25, 2016 na Desemba 30, 2016 saa 4:00
asubuhi, bibi huyo alimkeketa na baada ya kitendo hicho hali ya mtoto
ilikuwa mbaya kutokana na kutokwa na damu nyingi sehemu zake za siri,”
alisema Mutafungwa.
Mutafungwa alisema ilipofika Januari 11, 2017 mtoto huyo alifikishwa
katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC akiwa na mama yake mzazi, Fatina
Joshua (14).
Alisema baada ya kufikishwa hospitalini hapo madaktari waliompokea
walimkagua na kukuta mtoto huyo akiwa ameharibika vibaya sehemu zake za
siri na ilipofika Januari 13, mwaka huu alifariki dunia.
Kamanda Mutafungwa, alisema baada ya kupata taarifa hiyo waliwatafuta
watuhumiwa na kumkamata bibi pamoja na mama wa kichanga hicho.
Alisema mwili wa kichanga hicho umehifadhiwa katika Hospitali ya
Rufaa ya KCMC huku uchunguzi ukiendelea ili kuchukua hatua zaidi za
kisheria.
Aidha, Kamanda Mutafungwa alisema jeshi hilo pia linaendelea
kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Manyara kutokana na tukio hilo
kufanyika huko.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK