Acha Papara, Usikubali Wakuachie Majuto..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


NINA hasira kama nini hapa mnaponiona, yaani nimevurugwa kabisa. Mwenyewe nilijua timu yangu ndiyo tunachukua ubingwa msimu huu, mara eti katimu hakana hata historia na huu mchezo kamekuja kutuvurugia. Tangu siku ile sijatoka ndani, maana jirani yangu alikuwa ameweka madebe barazani anapiga ananisubiri! Kama siyo shoga yangu Ma Muhaji kuja nidokeza kisa cha mke wa rafiki wa mwanaye wa kiume, basi nilitaka leo niahirishe hili somo, nikae zangu ndani niendelee kusikilizia maumivu, yanaumajeee!!

Basi, Mama Muhaji kaniambia, eti mke wa rafiki wa mwanaye kaondoka nyumbani kwa ngoma, yaani kajaza watu akimtukana mumewe, matusi makubwamakubwa na watu wanashangilia. Kijana wa watu, nasikia kakaa kimya ndani, kavumilia mvua ya matusi na dharau, mwisho wa siku huyo dada kachukua begi lake, akaondoka kwa mbwembwe, eti wataonana kuzimu! Sasa alichonishangaza shosti, eti huyo bi dada kakaa huko alikokaa wiki tatu tu, karudi anataka waendelee na maisha na kijana wa watu.

Kilichonifurahisha, mvulana kamwambia mkewe, yupo tayari kuendelea kuishi naye ili mradi tu, ajaze watu kama alivyofanya siku ile anaondoka, halafu awaambie kwa nyodo zilezile kwamba anataka kurudi! Fyuutu, unadhani aliweza, akaishia kulialia na hadi jana anaondoka hapa kwangu Ma Muhaji, hata hatujui nini kinaendelea, maana mjumbe kakataa kwenda kusuluhisha, majirani wote hawataki na marafiki ndiyo kabisaa, wenyewe kwanza wanaona aibu wakikumbuka shoga yao alivyokuwa akitamba kwa pozi siku ile! Sasa kwa sababu hiyo ndo nimeona acha niwape kidogo uzoefu, maana nyie wengine mnadhani kubadilisha wanaume, au kuwa wajeuri ndiyo mnaonekana wajanja.

Kwanza shurti mjue, siku zote, pamoja na uzuri walionao, shepu zao na hata majukumu yao, heshima ya mwanamke inatokana na mwanaume. Asikudanganye mtu, achilia mbali kuolewa, ile tu kuishi na mwanaume ndani, ni heshima tosha kwa mwanamke.

Ile inakuonyesha ni kwa kiasi gani wewe una baraka za Mwenyezi Mungu, kwa sababu kuna wanawake na uzuri wao, hakuna mwanaume anafikiria kuishi nao. Na wasikudanganye ukisikia wanasema hawana shida na mwanaume, ni waongo. Mwanamke na hata awe na hela vipi, anaweza kutoka kwenye jumba lake la kifahari, akamfuata mwanaume anayeishi mbavu za mbwa.

Ukimpata mwanaume, shikamana naye. Usije kufanya jambo kwa sababu ya kutaka sifa kutoka kwa mashoga. Kwanza katika hao mashoga wanaoshangilia unapomkosea adabu mwanaume wako, wangapi wanaishi na wanaume? Mwanamke anayeishi na mume, hawezi kukuunga mkono kwenye ujinga huo, labda na yeye awe hamnazo! Kitu kingine ambacho sisi wanawake tunakuwa hatujui ni kwamba wenzetu wanaume, hata waache wanawake mara ngapi, hata hawaonekani kuwa na dosari, lakini sisi sasa, eti umeachika mara tatu tu, nakuambia hata kosa si lako utaonekana wewe ndiyo tatizo! Ninachotaka mjue, kile kitendo tu cha mwanaume kukubali kukuweka ndani, ni heshima kubwa sana.

Kuna maelfu ya mashoga huko mitaani wameshindwa kuwapata, tena wadada wazuri, wanajiremba, wanavaa, lakini ndiyo wanaishia maisha ya klabu, kila mwanaume anaguna ukimuambia amuweke ndani! Cha msingi, ukimpata, kaa naye chini mrekebishane makosa, lakini jivunie kuwa naye! Kwa leo ni hayo tu mashosti, tukutane wiki ijayo ni mimi Anti Nasra, Shangingi Mstaafu!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kwa kweli wewe Shangingi Mstaafu nimekuvulia kofia. Yani ni ukweli mtupu. Mangurubande kibaaaaaoooo huko mitaaani lakini yanajihangaisha tu. Leo kwa bwana huyu kesho yule lol hahahahahahahahahahahahaha aaaaaaaaaaahhhhhhhhhhh

    ReplyDelete

Top Post Ad