Serikali - Uzalishaji wa Chakula Nchini Utafikia Tani Milioni 3..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


SERIKALI imefanya tathmini ya awali ya uzalishaji wa mazao ya chakula nchini na kubaini kwamba uzalishaji wa chakula nchini utakuwa na ziada ya tani 3,013,515.

Akisoma kauli ya serikali kuhusu hali ya chakula na lishe nchini katika mwaka 2016/17 bungeni Dodoma jana, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Dk Charles Tizeba alisema tathimini iliyofanywa, imebaini kwamba jumla ya tani 35,491 za chakula zinahitajika katika kukabiliana na hali ya upungufu wa chakula na lishe kati ya Februari na Aprili mwaka huu kwa ajili ya watu 1,186,028 walioainishwa kuwa na upungufu katika halmashauri 55.

Kwa mujibu wa Dk Tizeba, ziada hiyo ilibainika baada ya Bunge la 10 kutoa kauli ya kufanya tathmini ya upatikanaji na mahitaji ya chakula ambapo tathmini ya awali ya uzalishaji chakula kwa mwaka 2015/16 na upatikanaji wa chakula mwaka 2016/17, ilikamilika.

Alieleza kuwa tathmini hiyo ilionesha kuwa kitaifa, uzalishaji wa chakula utafikia tani 16,172,841 za chakula na mahitaji ya chakula kwa mwaka huo ni tani 13,159,326 na hivyo kuwa na chakula cha ziada cha tani 3,013,515 yaani tani 1,101,341 ni mazao ya nafaka na tani 1,912, 174 ni za mazao yasiyo ya nafaka.

Aliongeza kuwa nchi ilikuwa na utoshelevu wa chakula kwa asilimia 123, lakini pamoja na hali nzuri cha chakula kitaifa, kulikuwa na halmashauri 43 ambazo zilikuwa na maeneo yenye upungufu wa chakula.

Aliongeza kuwa tathmini hiyo ilishirikisha Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) na Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) na Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) pamoja na Wizara ya Afya kupitia Taasisi ya Chakula na Lishe (TFNC).

Alieleza kuwa tathmini hiyo ilizingatia mihimili minne ya usalama wa chakula ambayo ni upatikanaji wa chakula, ufikiwaji wa chakula, utumiaji wa chakula na uthibiti wa chakula, ilitumia mfumo wa uainishaji madaraja ya usalama wa chakula na lishe.

Aidha, alisema Serikali inafuatilia mwenendo wa bei za mazao ya chakula hususani mahindi, mchele na maharage ili kujiridhisha uwepo wake sokoni.

Tathmini imebaini jumla ya tani 35,491 za chakula zinahitajika katika kukabiliana na hali ya upungufu wa chakula na lishe kati ya Februari na Aprili mwaka huu kwa ajili ya watu 1,186,028 walioainishwa kuwa na upungufu katika halmashauri 55. Aidha, watu 118,603 wasio na uwezo wa kupata chakula watahitaji tani 3,549 za chakula cha bei nafuu haraka.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad