AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Katazo hilo itaziathiri baadhi ya TV za mtandaoni zenye umaarufu ikiwemo Ayo TV ya Millard Ayo. Akiongea bungeni leo mjini Dodoma, Mbilinyi amedai kuwa uamuzi huo unaliingiza taifa gizani.
“Tunakuwa North Korea kwa spidi ya ajabu sana,” amesema.
“Tunaonekana wa ajabu kwenye international community kwa maamuzi kama haya. Kwasababu wananchi wana haki ya kupata habari kutoka upande wa pili, mfano jana Askofu Gwajima na mfanyabiashara Manji walipata nafasi ya kujibu kwa haraka sana tuhuma dhidi yao zilizotangazwa kwenye TV pendwa za serikali lakini wao wasingeweza kupata nafasi ya live kusingekuwa na online TV wakaweza kujitetea kwa haraka sana,” ameeleza.
“Wananchi sasa wamekuwa wakitegemea online TV kupata habari za bunge kwahiyo ni wazi suala la kuzuia kwa namna yoyote online TV ni mwendelezo wa kuzuia wananchi kupata habari za bunge, ni mwendelezo wa kuliweka taifa gizani.”
Sugu amependekeza kazi za online TV ziendelee hadi pale sheria hizo zitakapotungwa kwasababu uwepo wake hakuvunji sheria yoyote.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK