Wazo la Wimbo ‘Niambie’ Nilitaka Wolper Aniambie Kwanini Ananipenda – Harmonize...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize amedai idea ya wimbo wake mpya ‘Niambie’ ilitokana na aliyekuwa mpenzi wake, Jacqueline Wolper.

Muimbaji huyo amedai alishindwa kujua ni kwanini malkia huyo wa filamu alimpenda na kuwatosa wenye pesa zao ambao walikuwa wanamnyapia nyapia.

“Watu wamekuwa wakisema hatuendani mimi na Wolper huenda kwa sababu yeye alianza kuwa staa kabla yangu wakati huo nikiwa kijijini au hatuendani kwa kuwa yeye anapesa nyingi pengine kuliko mimi!,” Harmonize aliiambia Global TV Online.

Aliongeza, “Licha ya hayo yote lakini alikuwa ananionesha ananikubali, kunifanya niwe mwanaume hata kunitangaza kwenye jamiii. So sometime nikiwa nazi-appreciate zile treatment anazonipa kwa sababu wengi wenye pesa walikuwa wanamtaka. So nikapata idea ningependa siku moja uniambie kitu ambacho kinakufanya mimi unipende wakati mimi sina chochote,”

Wimbo huo mpya wa muimbaji huyo unapatikana kwenye mtandao wa www.wasafi.com.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad