Ameibuka Tena..Makonda Afunguka Juu ya Ufisadi Mzito wa Bilioni 7 za Serikali..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amefunguka kuzungumzia namna ambavyo baadhi ya watu walivyotaka kupiga Tsh Bilioni 7 za serikali kwa kutaka kuwalipa watu hewa fidia za kupisha maeneo yao kwajili ya maendeleo ya miradi mbalimbali ya serikali.

Aidha RC Makonda ameiagiza TAKUKURU kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua watu ambao wamehusika katika sakata hilo.

Akiongea na waandishi wa habari Jumanne hii ofisini kwake jijini Dar es salaam, RC Makonda amesema amepewa jukumu na Rais Magufuli la kusimamia hela ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali kwajili ya maendeleo ya miradi mbalimbali ndani ya mkoa wa Dar es salaam.

“Mh Rais kama alivyoagiza na kuelekeza kwamba kila pesa inayotoka itoke kulingana na malipo halali. Mimi kama mkuu wa mkoa ninayo majukumu mengi ambapo moja wapo ni kusaini vitabu vya wananchi ambao wanakwenda kulipwa fidia katika maeneo mbalimbali ambako miradi inapita. 

Katika miradi ya DMDP ambayo inahusika na barabara, ujenzi wa mifereji na uboreshaji mji wa Dar es salaam. Katika vitabu ambavyo nilitakiwa kusaini kwajili ya kupitisha hizo fedha zaidi ya tsh biloni 10 vilikuwa vitabu 31, lakini katika uchunguzi wangu na team yangu nikagundua vitabu 8 zimekiuka taratibu mbalimbali na masharti, na watu hao hawastahili kulipwa, na katika bilioni kumi tumebaini zaidi ya bilioni 5 na milioni 700 ni fedha ambazo zilikuwa zinaenda kulipwa kwa watu hewa,” alisema RC Makonda.

Alisema katika wilaya Kinondoni kati ya tsh bilioni 6 na tsh milioni 600, zaidi ya tsh bilioni 1 na tsh milioni 800 zilikuwa zinaenda kulipwa kwa watu wasiostahili.

RC Makonda amedai katika jambo ambalo lilimshangaza kampuni ya mafuta ilipewa kazi ya kuthamini majengo na ardhi jambo ambalo lipo kinyume na taratibu.

Alisema katika taarifa ambapo alipewa aligundua kuna mtu alitakiwa kulipwa tsh milioni 4 kwajili ya shimo lake la taka.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hapa kazi tu. Makonda pita gazi. Achana na hii ngozi nyeusi mpaka roho zao nyeusi, hawana hata uruma na wenzao.

    ReplyDelete

Top Post Ad