Jerry Muro: “TFF wanatugawa ili watutawale”

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Afisa Habari wa zamani wa Yanga Jerry Muro amedai kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania TFF linawagawa mashabiki wa mchezo huo nchini ili liwatawale. 

Muro amesema kuwa kitendo cha TFF kumfungia yeye pamoja na Afisa Habari wa Simba Haji S. Manara ni kwa sababu Shirikisho hilo linajaribu kuwagawa wapenda mpira Tanzania ili liwatawale vizuri. 

Akizungumza kwenye Clouds 360 ya Clouds TV April 29, 2017 Muro ameweka wazi kuwa atarudi katika nafasi yake katika klabu ya Yanga mara tu atakapomaliza adhabu yake, akisema: “Yah! Mimi ni mwanachama wa Yanga tangu nikiwa mdogo. Nilipokuwa Yanga, nilikuwa nafanya kazi zangu kama kawaida na Yanga siondoki. Akili ndogo inapokuambia kaa pembeni, unakaa pembeni kwa sababu akili kubwa haiwezi kupambana na akili ndogo. 

“Nilipofungiwa mimi, niliwaambiwa mashabiki tupambane nisifungiwe hawa watu wanatugawanya. Leo wananifungia mimi, kesho watamfungia Manara. Marana amefungiwa, wametugawanya na wanatutawala. Ndio maana nasema, tusikubali akili ndogo kuongoza akili kubwa. 

“Unaponiondoa mimi na Haji kwenye mpira, mbadala ni nani? Sisi tumeingia kwenye mpira, mpira ulikuwa umepooza. Tumepandisha morari kwenye mpira, tumeinua hamasa. Zile nafasi zipo kwa ajili yetu ndio maana tangu nimeondoka Yanga, nani amevaa viatu vyangu?” – Jerry Muro.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad