Baada ya Kudai Kuwa Anapokea Vitisho Vingi Juu ya Miasha Yake.Nay Ageukia Ufugaji wa Kuku!.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KUFUATIA mambo mengi kumtokea Mwanamuziki Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ tangu aachie wimbo wake wa Wapo, jamaa ameamua kubadilisha mfumo wa maisha yake ya kila siku.

Utakumbuka hivi karibuni NaY alielezea vitisho vya kuuawa anavyovipata kutoka kwa watu wasiojulikana ambao wanaonesha kutofurahishwa na tamko la Rais Dk. John Magufuli la kutaka aachiwe licha ya wimbo wake kuonekana una ukakasi.

Hata hivyo, kufuatia tukio hilo, dizaini kama jamaa ameamua kutojichanganya sana kitaa, badala yake inadaiwa na watu wake wa karibu kuwa, amekuwa akitulia nyumbani kwake akifanya shughuli za hapa na pale ikiwa ni pamoja na kufuga kuku wake wa kienyeji.

Kusikia hivyo, mapaparazi wetuwakamfungia safari hadi nyumbani kwake, Kimara Mwisho jijini Dar ambapo katika hali ya kushangaza, palikuwa pametawaliwa na ukimya ndipo baadaye ikabainika kuwa, watu aliokuwa anaishi nao akiwemo mama yake, wameondoka kwa hofu ya kufanyiziwa.

HUYU HAPA NAY Baada ya kubisha hodi kwa muda mrefu, alifi ka getini kijana mmoja ambaye kabla ya kufungua aliuliza maswali kibao ndipo alipokwenda kumuita baba mwenye nyumba (Nay).

Alipokuja Nay na kuona ni waandishi anaowafahamu akafungua. Akizungumzia maisha yake kwa sasa, msanii huyo alisema:

“Ni kweli hali yangu ya usalama haipo vizuri, sasa ili kujiepusha na mambo mengine inanilazimu kukaa nyumbani muda mwingi na kufanya shughuli kama hizi za kulisha kuku wangu, kuhudumia garden na shughuli nyingie ndogondogo.

“Kwa kifupi mimi ni mfugaji mzuri sana wa kuku wa kienyeji, ninao wengi na wamenizoea kwa kuwa ni wa kienyeji lakini nawalisha kizungu kama unavyoona.”
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad