AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
OFISA Habari wa Simba, Haji Manara, amewakoroga mashabiki na wanachama wa klabu hiyo kwa kitendo chake cha kutumia ukurasa wake wa Facebook ‘kuposti’ masuala ya siasa badala ya soka.
Juzi jioni Manara alitumia ukurasa wa Facebook kuandika ujumbe ambao ulikuwa unahusu Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiongelea masuala mbalimbali kuhusiana na uchaguzi ukiwamo wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki.
Wachangiaji wengi wa ukurasa huo ambao kwa asilimia kubwa ni mashabiki wa Simba, walionekana kutopendezwa na andiko hilo, kwani hawapendi kuchanganya masuala ya soka na siasa.
Miongoni mwa wachangiaji hao ni Juma Sayyed Bury ambaye aliandika: “Unatujaribu wewe, mambo ya vyama wapi na wapi? Acha mambo ya CCM wewe leta habari za Simba.
Shabiki mwingine aliyejulikana kwa jina la Sovezsck Kwangaiyya, alianza kwa mshangao: “Aaaaah! Haji hapa si mahali pake, binafsi sipendi siasa kabisa, ushauri wa bure ninaoweza kukupatia habari kama hii ya CCM iwasilishe katika ukurasa wao au makao makuu ya chama hicho Lumumba ilipozaliwa Tanu.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK