Kimenukaa..Ray C Apanga Kuvamia Radio Station Kama Alivyofanya Makonda..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya ukimya wa miaka kadhaa na misukosuko aliyopitia, Ray C ameweka wazi mpango wake wa kuyateka tena mawimbi ya radio na vituo vya runinga kwa kuachia mzigo wenye ujazo kamili.

Mwimbaji huyo ambaye tangu mwaka jana alikuwa akipost picha kadhaa kwenye mitandao ya kijamii akiwa studio, amefunguka kupitia Twenzetu ya 100.5 Times Fm kuwa tayari ameshapika nyimbo nane ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya albam yake.

Hata hivyo, Ray C amedai kuwa hajaridhika na nyimbo zote alizofanya hivyo ataendelea kurekodi kabla ya kuanza kurusha makombora mfululizo yakifuatiwa na albam hiyo.

“Hata hivyo bado sijaridhika ni nyimbo gani nitoe kwa sababu bado nilizokuwa nazo sijaridhika kwa sababu nimekulia katika maisha ya kutoa nyimbo kumi au kumi na tano halafu ndio natoa wimbo mmoja [kwanza], sijazoea kurekodi wimbo mmoja halafu nikaharakisha kutoa,” alisema Ray C.

Aliongeza kuwa anachofanya ni kuhakikisha anapata nyimbo tano bora zaidi zitakazochuana kila atakapokuwa akiziachia na kwamba kila siku anapoingia studio hujikuta akirekodi wimbo mkali zaidi ya uliopita, ndio sababu ya kutaka kuongeza nyingine.

‘Kiuno Bila Mfupa’ alidai kuwa anatarajia kuiza albam yake na kuiuza duniani kote kupitia mtandao.

Hivi karibuni, Ray C aliwaonjesha mashabiki wake ladha ya sauti yake kwa kurudia wimbo wa Recho ‘Upepo’ na kudhihirisha kuwa bado ana uwezo mkubwa.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad