Maswali Zaidi ya 1000 Yakosa Majibu Kuhusu Kutekwa na Kuachiwa kwa Roma Mkatoliki ..!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Yanaweza yakafika maswali 1,000. Mijini na vijijini watu wanajiuliza maswali na kama kila swali litachukuliwa kwa uzito, Roma Mkatoliki atakuwa na kazi ya kujibu zaidi ya maswali 1,000 ya Watanzania.

Baadhi ya maswali  ambayo hayajapata majibu kuhusu utekaji wa Roma ni pamoja na alichohojiwa na watekaji, kwa nini watekaji waliwafunga vitambaa vyeusi, kwa nini ofisa mmoja wa Serikali alitabiri kuwa watarudi kabla ya Jumapili na utata kuhusu mazingira ya kufika polisi baada ya kutekwa.

Siku moja baada ya kuachiwa na watekaji, Roma hakueleza alichohojiwa na watekaji. “Watekaji walikuwa wakituhoji na kutupiga,” alisema Roma aliyekuwa amefuatana na wasanii aliotekwa nao, Moni, Bin Laden na Imma.

Mchambuzi wa masuala ya siasa na jamii, Godlisten Malisa ameandika katika mtandao wake wa facebook akihoji maswali kadhaa kuhusu utekaji wa Roma.

Miongoni mwake anahoji, ni kwa nini msanii huyo alijikuta yupo Ununio, lakini akaenda kuripoti Kituo cha Polisi Kati (kikuu) na baadaye Oysterbay huku akiwa tayari amekwenda nyumbani kwake kubadilisha nguo ambazo ni ushahidi badala ya kwenda polisi moja kwa moja.

Swali hilo ambalo majibu yake hayajapatikana linapewa nguvu na idadi ya vituo vya polisi vilivyopo kati ya Ununio na Posta, ambayo Roma alivipita bila kujisalimisha na kutoa taarifa kuwa alikuwa ametekwa.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kama alikatazwa kusema mbona anasema ovyo na aseme alichofanyiwa basi au anaharibu majina ya watu na seeikali

    ReplyDelete

Top Post Ad