MWALIMU wa Shule ya Msingi Amuua Mwanaye kwa Kipigo..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Polisi mkoani Mwanza inamshikilia mwalimu wa Shule ya Msingi Mwamakoye wilayani Kwimba kwa tuhuma za kumchapa mtoto wake na kusababisha kifo chake.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alisema tukio hilo lilitokea Aprili 21 mwaka huu, saa kumi jioni na kumtaja marehemu kuwa ni Sifael Emmanuel (8) mwanafunzi wa shule hiyo.

Msangi alisema taarifa zilizopatikana zinasema kuwa, mtoto huyo alikuwa na tabia ya kuchelewa kurudi nyumbani pindi anapoagizwa dukani na mama yake.

“Kutokana na tabia hiyo mama yake alikuwa akimpatia adhabu, lakini hakukoma na kwamba juzi mtoto huyo aliagizwa tena dukani na kuendelea na tabia yake ileile,” alisema.

Kamanda alieleza zaidi kuwa mtoto huyo aliporejea kutoka dukani, baba yake alimshika na kuanza kumshushia kipigo kwa muda mrefu.

“Wakati anaendelea kumpiga, mtoto alikuwa akilia na akaishiwa nguvu na baada ya muda mfupi akapoteza maisha,” alisema Msangi

Kutokana na tukio hilo, wananchi walioshuhudia walitoa taarifa kituo cha polisi na baadaye mwalimu huyo alikamatwa na kupelekwa kituoni.

Aliongeza kuwa kwa sasa baba wa mtoto huyo anahojiwa na polisi hadi uchunguzi utakapokamilika na atafikishwa mahakamani.

Pia, Msangi alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kwimba kwa ajili ya uchunguzi na kwamba, utakapokamilika utakabidhiwa kwa ndugu kwa ajili ya mazishi.

Kamanda huyo aliwaonya baadhi ya wazazi wanaowafundisha watoto wao kwa kuwachapa na fimbo huku akiwataka kutumia namna nyingine ya kuwaelekeza wanao.

Vilevile, alishauri kuwa ni vyema zaidi kuwaonya watoto kwa maneno ya hekima au vitabu vya dini ili kuepuka adhabu zinazoweza kuleta madhara.

Akizungumzia tabia ya baadhi ya wazazi kuwaadhibu watoto wao kwa kuwachapa fimbo, mkazi wa Nyamanoro, Amina Lusheshu alisema ni vyema adhabu ikatolewa kwa kuzingatia umri.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad