AJABU: Njemba Yafunga Ndoa na ‘Simu Yake’ Kanisani..!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Dunia ina mambo, na ukiyashangaa haya jiandae kuyastaajabia yajayo..!

Mwanaume mmoja aliyejitambusha kwa jina la Aaron Chervenak mwenye umri wa miaka 34 na mkazi wa Los Angeles nchini Marekani, amefanya tukio la aina yake baada ya kufunga ndoa kanisani na simu yake ya kupapasa (smartphone).

Mwanaume huyo alisafiri hadi Vegas kulisaka kanisa moja ambalo lilimkubalia kufunga ndoa na simu yake na kula kiapo kama ambavyo alipaswa kula kiapo kwa mrembo aliyeyagusa maisha yake na kuamua kumfanya mkewe wa maisha.

Akizungumzia sababu zilizopelekea yeye kufanya tukio hilo, kupitia makala maalum ya ndoa yake hiyo, Aaron alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa sababu ya ukweli kwamba simu zimekuwa zikichukua nafasi kubwa ya mapenzi na uhusiano na zikifanya jukumu kubwa la kuwatuliza watu katika dunia hii.
“Kama tutakuwa wakweli, tunaunganishwa na simu katika viwango vingi vya hisia. Tunaikimbilia kututuliza, kutulaza usingizi, kuweka unafuu kwenye mawazo yetu. Na kwangu, huo ndio uhusiano nilionao na simu yangu hii,” alisema Aaron.

“Kwa mantiki hiyo, simu yangu hii imekuwa na uhusiano wa muda mrefu na mimi na ndio maana nimeamua kufunga nayo ndoa,” aliongeza.

Kuhusu jinsi alivyokubaliwa kufanya tukio hilo kanisani, alisema kuwa alijaribu kuwasiliana na uongozi wa kanisa hilo kuona kama angeruhusiwa lakini alihakikishiwa kuwa anakaribishwa kwa mikono miwili.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad