AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msanii wa hip hop, Kala Jeremiah amemuomba Waziri Mwakyembe kutengua kauli yake ya kuwataka wasanii waache kuimba nyimbo zinazohusu siasa, kwa madai kuwa ni kuwatenga mbali na jamii inayotegemea wasanii kuwasemea mahitaji yao.
Akizungumza kwenye 'story' tatu ndani ya Planet Bongo, Kala amesema kuwa kauli ya Mh. Mwakyembe haiko sawa kwani inatengeneza 'gap' kubwa kati ya jamii na wasanii na kuongeza kwamba siasa zinazoimbwa na wasanii ndizo ambazo zinasaidia jamii na wakati mwingine zinasaidia serikali kutopoteza pesa.
Aidha Kala amendelea kufunguka kwamba yeye kama msanii anayeimba harakati kwa ajili ya kusaidia jamii yake kauli ya Waziri ni kama inamlazimisha kuimba nyimbo za mapenzi kitu ambacho kwake hakitampa tatizo lakini hasara itakuwa kwa jamii inayohitaji kusemewa.
Pamoja na hayo Kala amefunguka na kusema wimbo wake alioimba kuwasemea watoto yatima 'Wanandoto' umempatia sifa kubwa kutoka kwenye mashirika mbalimbali yanayojihusisha na kusaidia watu wenye matatizo na kumpongeza kwa kuweza kufikisha ujumbe mzito pasipo kutumia gharama kubwa sana.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK