CHADEMA Watoa Tamko Hili Baada ya Uchaguzi wa Wabunge wa Afrika Mashariki Jana..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimewapongeza wabunge wake wateule wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala).

Wabunge waliochaguliwa na Bunge la Tanzania kutoka kundi C ni Josephine Lamoyan na Pamela Maassay.

Chadema imesema ina imani kubwa kuwa wabunge hao wateule wa Eala watakuwa wawakilishi bora wa nchi kwenye Bunge hilo wakizingatia manufaa, masilahi na matakwa ya Watanzania na wananchi wa nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Taarifa ya pongezi ya Chadema inasema kupitia uwezo, uzoefu na u-tayari walionao wa kujifunza na kupokea maarifa mapya; Lemoyan na Maassay watabeba matumaini ya mabadiliko ya Watanzania, ambao wangependa kuona ushirikiano wa EAC unakuwa na nguvu za kiuchumi na kisiasa uliojengwa katika misingi ya kidemokrasia kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wananchi.

“Chama kinawaahidi ushirikiano wakati wowote watakapohitaji ili waweze kutimiza wajibu na majukumu hayo kwenye uwakilishi wa Eala na EAC kwa jumla kwa niaba ya nchi yetu,” imesema taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Chadema Tumaini Makene baada ya uchaguzi uliofanyika jana (Jumatano).
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad