AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Halima Mdee amesema hayo bungeni leo wakati akichangia katika bajeti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi baada ya wabunge wengi wa Chama Cha Mapinduzi kusimama na kuanza kusifia Wizara hiyo kuwa imepiga hatua baada ya kufuta tozo nyingi jambo ambalo Halima Mdee anasema ni jambo dogo sana ukilinganisha na changamoto ilizonazo Wizara hiyo ambayo kila mwaka imeonekana kushuka katika sekta ya kilimo ambacho ndiyo uti wa mgongo wa taifa.
Kufuatia jambo hilo Halima Mdee amewataka wabunge wa CCM kusoma vizuri Ilani ya Uchaguzi waone inasema nini na inataka nini lakini pia wasome na mpango wa maendeleo ili kuona changamoto ambayo Wizara hiyo inayo.
"Nimeona wabunge wengi vijana hata wale watu wazima wakisimama na kutoa pongezi kwa Waziri kisa tu amepunguza tozo, lakini ndugu zangu tozo pekee ni kitu kidogo sana lakini hata Waziri alitumia muda wake mwingi jana kuhusiana na tozo tu, ndugu zangu Wabunge wa CCM mkasome vizuri Ilani ya Uchaguzi ya CCM, mkasome na mpango wa maendeleo, hapa hatutafutiani ubaya kwani mafanikio yenu nyinyi ndiyo mafanikio yetu sisi pia, kwa hiyo tusichukiane tunasema haya kwa dhamira njema, ukichukua kitabu cha Wizara ya Kilimo na kile cha Wizara ya Viwanda haviendani yaani ni kama mbigu na dunia" alisema Halima Mdee
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK