IMEJULIKANA ..Ray C Ataka Kujiua Mara 10

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MWANAMUZIKI ambaye miaka kadhaa iliyopita alipotea kwenye anga la muziki baada ya kujitumbukiza kwenye matumizi ya madawa ya kulevya, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amefunguka jinsi alivyotaka kujiua zaidi ya mara 10 kutokana na kujichukia.

Akizungumza na Wikienda katika mahojiano maalum wikiendi iliyopita, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kuwa, alifikia uamuzi huo mara kwa mara baada ya kujichukia kupita kiasi huku akiona kuwa hana thamani tena duniani wala hajui atatokaje kwenye dimbwi alilojiingiza akiwa bado msichana mdogo.

“Kujiua kwangu lilikuwa ni wazo la mara kwa mara, inaweza ikawa hata zaidi ya mara kumi kutokana na kukata tamaa kabisa ya maisha huku nikijitazama nilivyokuwa msichana mwenye ndoto nyingi lakini nateketea nikijiona,” alisema Ray C.

Mwanamuziki huyo ambaye amerejea kwenye gemu kwa kishindo alisema kuwa, nia ya kujitoa uhai ilikuwa ikitokana hasa na kuamini kwamba hawezi tena kujinasua sehemu aliyokwama kutokana na kujaa vizingiti vya kushindwa hivyo kufikiria hakuna njia nyingine zaidi ya kifo.


“Kuna wakati nilikata kabisa tamaa kuwa hakuna njia nyingine ya kunifanya nipumzike na tabu niliyokuwa nikipata zaidi ya kujitoa uhai ambao kwangu haukuwa na thamani na wala sikuwa ninajipenda tena hata kidogo,” alisema Ray C ambaye anatamba na wimbo wake mpya wa Unanimaliza.

By Imelda
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad