AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Bodi ya Ligi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imewajibu rasmi Simba SC juu ya sakata lao la kupokwa pointi tatu za mezani walizopewa baada ya rufaa yao dhidi ya Kagera Sugar wakidai kumcheza mchezaji Mohamed Fakhi akiwa na kadi tatu za njano.
Kwa mujibu wa barua kutoka katika Bodi ya Ligi zimesema kuwa Fakhi hakuwa na kadi tatu za njano wakati akicheza mchezo dhidi ya Simba uliofanyikia uwanja wa Kaitaba, Bukoba Aprili 2 mwaka huu.
"TFF ambayo ndiyo yenye dhamana ya usimamizi wa mpira nchini na ambayo ndiyo iliyokaimu madaraka kwa TPLB kuendesha ligi kuu iliitisha kikao cha Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ambayo ilichunguza kwa undani sakata hili na baada ya uchunguzi wao ambao walihoji watu mbalimbali, walituandikia kutujulisha kuwa wamebaini mchezaji Mohamed Fakhi anayelalamikiwa na Simba hakuwa na kadi 3 siku ya mchezo wa Kagera Sugara dhidi ya Simba hivyo alikuwa halali kucheza mchezo huo". Ilisema barua hiyo
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mpira uwanjani sio mezani
ReplyDelete