AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
WEKUNDU wa Msimbazi Simba wamejibu mapigo kwa wapinzani wao wa jadi, Yanga baada ya kumtaja beki wao mahiri, Kelvin Yondani na kiungo Haruna Niyonzima ambao mikataba yao inaelekea ukingoni.
Simba wamefanya hivyo kama sehemu ya kujibu mapigo kwa wapinzani wao hao ambao kila kukicha wamekuwa wakiwataja wachezaji wao mahiri, kiungo Jonas Mkude na mshambuliaji Ibrahim Ajib ambao nao wanamaliza mikataba.
Akizungumza na BINGWA, Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, alisema wapinzani wao Yanga waache kuwatoa kwenye reli ya ubingwa kwa sasa kwa kutaja nyota wao wanaotaka kuwasajili.
Alisema Yanga wanatakiwa kuwazungumzia nyota wao 14 wanaomaliza mikataba, akiwamo Haruna Niyonzima na Kelvin Yondani akidai kuwa ndio wenye uwezo wa kuichezea Singida United iliyopanda Ligi Kuu msimu huu.
“Kimsingi hata kifikra utaona kuwa si Yanga wala Singida United wenye uwezo wa kuwasajili akina Ajib, Mkude na Said Ndemla kwa kuwa tumeshamalizana nao, lakini pia tambua fika hawa hawawezi kwenda kucheza timu ya porini,” alisema Kaburu.
Alisema ni ngumu kwa nyota hao hivi sasa kuikacha Simba na kwenda kusaini Singida United kama ilivyokuwa ikiandikwa katika vyombo mbalimbali vya habari na kusisitiza kuwa bado wataendelea kukipiga kwa Wekundu hao wa Msimbazi.
Hatua ya nyota hao kutajwa katika usajili wa Singida United inakuja ikiwa ni siku chache tangu timu hiyo ipande Ligi Kuu na kupanga huku wakionekana kuwa na mikakati kabambe ya kutaka kuzinasa saini za wachezaji wengi nyota wa Ligi Kuu Bara, wakiwamo Ajib na Mkude.
Credit - Bingwa
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK