SUMAYE - Nimejiuzulu CRDB Bank Baada ya Familia Yangu Kufuatwafuatwa na Kuandamwa Kila Muda..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Aliyekuwa Waziri Mkuu wa serikali ya awamu ya tatu, Frederick Sumaye amejitoa katika Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB kwa madai kuwa familia yake inafuatwafuatwa hivyo kuhofia kuwa anaweza kuathiri benki hiyo.

Baada ya kujitoa kama mmoja wa viongozi wa benki hiyo kubwa nchini, Sumaye amesema kuwa ataendelea kuwa mwanahisa wa benki hiyo ya biashara.

“Sitaki msimamo wangu wa kisiasa uhusishwe na benki yetu” alisema Sumaye ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani.

Sumaye alisema kuwa huenda majukumu yake ya kisiasa yakambana na akashindwa kuhudhuria baadhi ya vikao muhimu vya benki hiyo ambavyo ni muhimu kwa ufanisi na ustawi wa benki.

Akiwa nje ya mkutano huo Sumaye alisema kuwa, familia yake imekuwa ikifuatwafuatwa na serikali na kwamba tayari mtoto wake amepokwa shamba.

Serikali pia alimnyang’anya Sumaye shamba lake lililokuwa Mabwepande kwa madai hakuliendeleza, huku yeye akisema uamuzi wa yeye kupokwa shamba ulikuwa ni wa kisiasa. Sumaye alieleza kwamba hakuweza kulima shamba hilo kutokana na serikali kupiga kilimo jijini Dar es Salaam.

Sumaye amesema uamuzi wake aliuchukua ili CRDB iweze kuendeshwa na watu walioko huru mbele ya jamii kuepusha hisa za wafanyabishara wengine kuathiriwa.

Sumaye anamiliki zaidi ya hisa milioni 7.4 za benki hiyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad