Kagame atangazwa kuwa mgombea Urais Rwanda

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katika hatua iliyowashangaza wengi nchini Rwanda vyama viwili vya siasa vikongwe nchini humo vimemtangaza Rais Paul Kagame kuwa mgombea wao katika uchaguzi wa urais utakaofanyika mwezi wa 8 mwaka huu, kabla hata chama chake cha RPF kumtangaza kuwa mgombea wake.

Hadi sasa ni wagombea binafsi 3 waliokwishatangaza nia ya kusimama katika uchaguzi huo.

Katika mikutano mikuu ya vyama hivyo, chama cha Social Democratic na Liberal Party licha ya kwamba ilifanyika mnamo nyakati tofauti, kauli yao ilikuwa moja, kuunga mkono Rais Paul Kagame wa chama tawala cha RPF katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwezi wa 8 mwaka huu.

Hoja iliyotolewa na vyama hivyo pia haitofautiani.

Ni kwamba chaguo lao limetokana na pendekezo lililoungwa mkono na wananchi wengi wa Rwanda la kubadili katiba na kumpa rais Paul Kagame uhuru wa kugombea muhula wa tatu kupitia kura ya maoni iliyopitisha katiba mpya mwaka jana.

Haya yametokea wakati ambapo hata chama tawala RPF hakijamtangaza Rais Paul Kagame kama mgombea wake, wakati mchakato wa uteuzi bado umekuwa ukiendelea katika ngazi ya mashinani.

Wengi walitarajia kuwa vyama hivi vingeteua na kutangaza wagombea wake katika uchaguzi huo kama ilivyotokea katika uchaguzi wa urais mwaka 2010.

Chama cha Social Democratic kilisimamiwa na Dr Jean Damascene Ntawukuriryayo aliyepata asilimia 4,9 ya kura ilhali Liberal Party kilisimamiwa na Higiro Prosper aliyeambulia asilimia 1 nukta 3 ya kura.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad