Profesa wa Kenya Amwagia Sifa Kedekede Rais Magufuli..Adai Akikaa Miaka 10 Madarkani Tz Itakuwa Juu Kiuchumi..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MWANATAALUMA kutoka nchini Kenya, Profesa Patrick Lumumba amesema kuwa endapo Rais John Magufuli ataendelea na jitihada za kupambana na ufisadi kwa miaka 10, uchumi wa Tanzania utakuwa juu.

Profesa Lumumba alisema jana kwenye Tamasha la Tisa la Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alipokuwa akizungumzia mwanasiasa kuinuka na kuanguka barani Afrika.

Katika maelezo yake, Profesa Lumumba alisema rushwa imeondoa afya barani Afrika, wanasiasa wanapoiacha ikawatawala inawaletea shida. Alisema kwa kipindi kifupi Rais Magufuli alipoingia madarakani, ameonesha njia kwa wanasiasa wengine barani Afrika, ambao wamekumbatia rushwa na kuwaacha wananchi.

“Magufuli ana pumzi ya hewa safi, kama ataendelea hivi baada ya miaka 10 uchumi wa Tanzania utakua juu. Mungu msaidie Rais John Magufuli,” alisema Profesa huyo. Kwa upande mwingine, alisema kuwa Afrika ni bara zuri na lenye uwezo, ila kilichofanyika kwa miaka 30 iliyopita kumekuwa na viongozi wabinafsi, lakini katika miaka ya sasa wameibuka viongozi wazalendo kama Magufuli, Rais Paul Kagame wa Rwanda, Rais Yoweri Museveni na wengineo.

“Viongozi kama hawa wakiungwa mkono na wananchi wazalendo, Afrika itapiga hatua,” alisema. Aliwataka waafrika wajue watambue kuwa umoja ni nguvu utengano ni udhaifu, hivyo ni jambo linalochukua muda mrefu. “Ni jambo lililonifurahisha kuwa Magufuli ametoa mafichoni watu waliohodhi mali zetu kwa muda mrefu na kukubali kulipa. Ni hatua nzuri inastahili kupongezwa,” alisema.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad