Walichochukua polisi nyumbani kwa Lissu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


 Baada ya jeshi la polisi kumkamata Tundu Lissu siku ya Alhamsi uwanja wa ndege akiwa anaelekea nchini Rwanda. Jana jeshi hilo lilikwenda kufanya upekuzi nyumbani kwa Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA) ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa chama hicho.

Siku ya jana Ijumaa ya tarehe 21/07/2017  jeshi la polisi walimchukua Tundu Lissu na kwenda naye mpaka kwa Mkemia Mkuu wakiwa na lengo la kutaka kumpima mkojo kabla ya kuelekea nyumbani kwake kufanya ukaguzi. Lakini kiongozi huyo aligoma kufanya kipimo hicho kwa madai kuwa tuhuma anazotuhiwa haziendani na vipimo hivyo.

Kwa mujibu wa Tumaini Makene ambaye ni Afisa habari wa (CHADEMA) anasema kuwa jana polisi baada ya kufanya ukaguzi nyumbani kwa Tundu Lissu waliweza kuchukua CD 6 na kuondoka nazo. 

"Jeshi la Polisi bado linamshikilia, Mhe. Tundu Lissu, Kwenye upekuzi jana nyumbani kwake walichukua CD 6 za 1996 zinazohusu masuala ya mgodi wa Bulyag'hulu, Shinyanga" ilisema taarifa ya CHADEMA

Leo ni siku ya pili toka kiongozi huyo anashikiliwa na jeshi la polisi Dar es Salaam lakini Wakili Peter Kibatala pamoja na Wakili Fatma Karume wa IMMA Advocates kwa upande wao wanasema wanaendelea na juhudi za kisheria kuhakikisha kiongozi huyo anapatiwa dhamana au kufikishwa mahakamani mapema iwezekanavyo.


Source: Eatv
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad